Mchezo
wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Yanga SC na JKT Ruvu
uliokuwa ufanyike Jumatano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam umeahirishwa.
Mchezo huo uliopangwa kuchezwa Jumatano
ya Agosti 31 sasa utapangiwa tarehe nyingine. Na hatua hyo inatokana na
Yanga kuomba uahirishwe kwa sababu ina wachezaji wengi katika kikosi cha
timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars. Wachezaji hao ni pamoja na Kipa
Deogratius Munishi ‘Dida’, mabeki Vincent Andrew ‘Dante’, Kelvin
Yondani na Mwinyi Hajji, kiungo Juma Mahadhi na mshambuliaji Simon
Msuva.
Aidha, Yanga pia imesema wachezaji wake
wengine, beki Vincent Bossou (Togo), kiungo Haruna Niyonzima (Rwanda) na
mshambuliaji Amissi Tambwe (Burundi) nao pia wameitwa na timu zao za
taifa na kufanya idadi ya wachezaji wanane kutokuwepo siku hiyo.
Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara zinaruhusu timu ambayo wachezaji wake wasiopungua watano wameitwa
timu za taifa kuahirishiwa mechi.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles
Boniface Mkwasa ameita wachezaji 20 watakaosafiri kwenda Nigeria kwa
ajili ya mchezo wa mwisho wa kukamilisha ratiba ya mechi za Kundi G
kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017).
Mbali na Dida, Yondani, Dante, Mngwali,
Mahadhi na Msuva wengine ni Aishi Manula, Mohamed Hussein, Shomari
Kapombe (Azam FC) na David Mwantika (Azam FC). Viungo ni Himid Mao (Azam
FC), Shiza Kichuya (Simba SC), Ibrahim Jeba (Mtibwa Sugar), Jonas Mkude
(Simba SC), Muzamil Yassin (Simba SC), na Farid Mussa (Teneriffe ya
Hispania). Washambuliaji ni Jamal Mnyate (Simba SC), Ibrahim Hajib
(Simba SC), John Bocco (Azam FC) na Mbwana Samatta – CK Genk ya
Ubelgiji.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment