September 09, 2016


  

Ukubwa wa deni la taifa siyo jambo linaloweza kusababisha kuyumba kwa uchumi wa nchi, kinachooneka ni kuendela kuaminiwa kwa Tanzania ndani na nje ya nchi jambo linalopelekea tuna pata fursa ya kukopesheka kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Mchambuzi wa masuala ya kiuchumi, Profesa Haji Semboja alipofanya mahojiano maalum na mwandishi kutoka Idara ya Habari, MAELEZO kuhusu hali ya uchumi ilivyo kutokana na ongezeko la deni la Taifa leo Jijini Dar es Salaam.

“Ukubwa wa deni la taifa siyo mzigo mbaya, ni mzigo wa kimaendeleo. Unnecessary devil” Alisema Profesa Semboja.

Aliongeza kuwa kutokana kwa imani waliyo nayo wahisani ndani na nje ya nchi ndiyo maana washirika wetu wanatukopesha fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama ambavyo tumeshuhudia ujenzi wa Daraja la Kigamboni, hivi karibuni tutanufaika na usafiri wa ndege”. Alisema Profesa Semboja.

Aidha amempongeza Rais wa Awamu ya Tano Mhe. Dkt. Jonh Pombe Joseph Magufuli kwa hatua alizochukua za kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuondoa safari za nje zisizo za rasmi pamoja na kupiga vita vitendo vya rushwa.

Semboja aliendelea kusema kuwa kinachofanyika hivi sasa ni Serikali ya awamu ya Tano kulipa madeni ya watangulizi wake huku ikitekeleza miradi ya maendeleo jambo linaloongeza imani miongoni mwa wahisani.

Hata hivyo alionya juu ya matumizi mabaya ya rasilimali fedha kuwa zinasababisha kushindwa kutekeleza wajibu wa kulipa deni kwa wakati na kupelekea kulimbikiza madeni jambo ambalo si sahihi.

Alitajaa baadhi ya matumizi mabaya ya fedha kuwa ni pamoja na safari za nje na ndani ya nchi zisizokuwa na tija, ulevi, kupelekea fedha katika miradi isiyopangwa na mengine.

Wananchi wametakiwa kutoyumbishwa na waelewi kuwa kupitia fedha zinazokopwa wanufaika wakuu ni wananchi wenyewe, mfano fedha zitakazo tumika kujenga Nyumba za Magomeni ambazo Mhe. Rais amehaidi waliokuwa wakazi wake kuishi bila kulipia kwa kipindi cha miaka mitano zikitokana na mikopo hiyo wananufaika.

Related Posts:

  • Bunge la ahirishwa, kisa Lipumba kukamatwa, UKAWA wakomali   Tukio hili limetokea leo hii Bungeni Dodoma baada ya wapinzani kutaka hoja binafsi ya kukamatwa kwa mwenyekiti wa CUF Prof. Lipumba katika maandamano jana   Mbatia alisimama na kutoa hoja ya dharura ijadil… Read More
  • Juma Kaseja kusomewa mashtaka Februeary 12    Baada ya Uongozi wa Klabu ya Yanga kutangaza kuachana na aliekuwa mlindamlango wake Juma Kaseja na baadae kumfungulia mashtaka katika Mahakama ya kazi , hatimaye mlind amlango huyo sasa anatarajia kusomewa … Read More
  • CUF- Waandamana leo. Prof Lipumba akamatwa na polisi  Leo January 27 2015 Chama cha wananchi Cuf- kimefanya maandamano ya kumbukumbu ya mauaji ya 2011 Visiwani Zanziba. Lakini katika maadhimisho hayo yameingia dosari baada ya viongozi wa ngazi za juu wa Cuf kukatwa na p… Read More
  • Wafanyan biashara Morogoro wagoma   Wafanya biashara mkoani Morogoro leo hii, wamegoma kufungua maduka na kuendelea na shughuli hiyo kutokana na mgomo unaoendelea.    Tukio hilo linaloendelea sasa ni kutokana na taarifa ya kukamatwa kwa … Read More
  • Hakuna wa kutembelea nyota yangu -Ray C    Mwanamuziki Ray C ambae alitamba miaka ya nyuma na ngoma kali kibao ikiwemo Na wewe milele,Sogea sogea na nyingine nyingi amefunguka na kusema kuwa kwa sasa hakuna mtu atakae weza kutembelea nyota yake katik… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE