September 09, 2016



taifa-stars-vs-nigeria1-2

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetuma salamu za shukrani kwa Gavana wa Jimbo la Akwa Ibom, Gabriel Emmanuel kwa zawadi ya dola za kimarekani 10,000, (sawa na Sh milioni 21.7) kwa timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania ‘Taifa Stars’,  baada ya kuonesha mchezo mzuri na wa upinzani dhidi ya wenyeji, Timu ya mpira Super Eagles ya Nigeria uliofanyika Uwanja wa Kimataifa wa Godswill Akpabo, mjini Uyo.
Taifa Stars ilicheza mechi hiyo siku ya Jumamosi Septemba 3, 2016 katika mchezo wa mwisho wa hatua za makundi kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017). Katika mchezo huo ambao mashabiki waliingia bure, Taifa Stars ilifungwa bao 1-0 licha ya kuibana Super Eagles kiasi cha kumfanya Gavana huyo kuandaa hafla ya chakula cha jioni (Dinner) ambako mbali ya kuizawadia kiasi hicho Taifa Stars, pia aliizawadia Super Eagles dola za kimarekani 35,000.
Taifa Stars ilitua Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo Septemba 5, 2016 ambako baadhi ya wachezaji walipelekwa Hoteli ya Urban Rose, iliyoko katikati ya Jiji la Dar es Salaam wakati wengine hususani wale wa timu ya Azam FC walichukuliwa na viongozi wao kwa ajili ya safari ya kwenda Mbeya ambako Jumatano wanatarajiwa kucheza na Tanzania Prisons kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaofanyika Uwanja wa Sokoine mjini humo.
Wakati nyota hao 18 wakiwa wamerudi Dar es Salaam, Nahodha wa timu hiyo, Mbwana Samatta aliishia Nairobi, Kenya ambako aliunganisha ndege ya kwenda Brussels, Ubelgiji anakocheza mpira.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE