September 09, 2016

1

Mbunge wa Singida Mashariki ambaye ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mwanasheia Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu akizungumza na wanahabari. (hawapo pichani)
 

MBUNGE wa Singida Mashariki ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,Tundu Lissu, amesema aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Iblahim Lipumba amekosa hoja ya kuzungumza na badala yake anawavuruga wanachama wa CUF.
Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema amesema Lipumba hakuwahi kuwa na idadi kubwa ya wabunge kama walivyo sasa tangu alipoanza kugombea urais zaidi ya kupata viti viwili tu lakini walipoungana mwaka jana katika umoja wao wa Ukawa wakaibuka  na viti 10.
Kauli hiyo ameisema leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wanahabari ambapo aliongeza kuwa Lipumba aache kukiandama Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa madai ya kuwa kinaivuruga CUF.
Aliongeza kuwa Lipumba kuendelea kutoa matamshi hayo kwa wanachama wa CUF ni chanzo cha yeye kuendelea kukivuruga chama hicho hivyo wanachama wampuuze kwani alikikimbia tokea walipoungana katika umoja wao wa Ukawa kabla ya mwezi mmoja kujiunga  aliyekuwa mgombe urais kupitia umoja huo, Edward Lowasa kupitia Chadema.
2 
Lissu akisikiliza kwa makini maswali aliyokuwa akiulizwa na wanahabari.
Kwa upande mwingine Lissu amesema viongozi wa Chadema wamepanga Jumanne wiki ijayo kupelekea malalamiko yao katika Mahakama Kuu ya Tanzania kwa ajili wafuasi 10 wa Chadema waliokamatwa kwa madai ya kusambaza maneno ya uchochezi.
3 
Viongozi hao wakiendelea kusikiliza maswali ya wanahabari yaliyokuwa yakiulizwa.
Alisema wanapeleka hoja hiyo mahakamani ili mahakama iweze kuamuru waachiwe huru kwani hivi sasa wanateseka mahabusu.
4 
Mkutano ukiendelea na wanahabari.
Alisema mahakama ndiyo chombo kikuu chenye dhamana ya kuwahoji Mkuu Jeshi la Polisi, IGP Ernest  Mangu na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini DCI, Diwan Athumani ili watoe sababu ya jeshi la polisi kuwaweka mahabusu wanachama 10 wa chadema kwa zaidi ya wiki moja sasa bila kuwapeleka mahakamani.

Related Posts:

  • Nuh Mziwanda atimua kwa Shilole Mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani umemfanya msanii wa Bongo Fleva,Nuh Mziwanda kuondoka nyumbani kwa mpenzi ambaye ni msanii,Shilole ili kumpisha mpenzi wake afunge kwani hawajafunga ndoa. Shilole ameyazungumza hay… Read More
  • Neymar apewa kadi nyekundu baada ya mechi   Nyota wa timu ya Brazil Neymar alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kipenga cha mwisho cha mechi ya kinyang'anyiro cha Copa America baada ya timu yake kufungwa na Colombia kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1991. Msh… Read More
  • Jicho letu October:Kwa nini Nyerere hana mrithi wa urais CCM ?   Ikiwa Tanzania inaeleke akatika tukio kubwa la ktaifa  Uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na rais, OCTOBER 2015. Hapa tunazidi kuwaletea Taarifa mbalimbali zinazohusiana na Uchaguzi mkuu.  Leo hii tuna… Read More
  • Wapinzani waipasua Serikali  Mwenyekiti wa maofisa watendaji wakuu wa makampuni, Ali Mufuruki (Kushoto) akiangalia kitabu cha Azimio la Tabora alilokabidhiwa na kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe (wa pili kushoto) baada ya kum… Read More
  • Idadi ya wasanii waliotangaza kugombea Ubunge 2015 hii hapa Muigizaji Wema Sepetu ametangaza kuwania Ubunge wa viti maalum Singida Wasanii wa filamu na muziki wameamua kujitokeza kuwania nafasi za ubunge katika maeneo mbalimbali nchini katika uchaguzi wa 2015. Mpaka sasa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE