October 31, 2016



Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza siku 90 kuanzia leo (Jumatatu, Oktoba 31, 2016) kwa waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2016/2017 kukata rufaa kwa njia ya mtandao ikiwa hawajaridhsihwa na matokeo ya upangaji uliotangazwa hivi karibuni.

Serikali imetenga Tshs 483 bilioni kwa ajili ya kutoa mikopo kwa jumla wanafunzi 119,012 – kati yao, wanafunzi 93,295 ni wanaondelea na masomo na wanafunzi 25,717 ni wa mwaka wa kwanza. Hadi sasa, jumla ya wanafunzi 20,183 wa mwaka wa kwanza wameshapata mikopo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo (Jumatatu, Oktoba 31, 2016) na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru, Bodi imeanza kupokea rufaa hizo kwa njia ya mtandao (Online Loan Application and Management System) kuanzia leo (Oktoba 31, 2016) hadi Januari 31, 2017.

“Wanachotakiwa kufanya wanafunzi ni kuingia katika mtandao wetu wa http://olas.heslb.go.tz na kujaza fomu, kuichapa na kuiwasilisha kwa Afisa Mikopo wa chuo chake ambaye atawasilisha kwetu fomu zote za chuo chake kwa barua kwa ajili ya sisi kuzifanyia kazi,” amesema Bw. Badru.

ANGALIZO: Ada ya Maombi ya Tshs 10,000/- iliyopaswa kulipwa na waombaji mikopo kwa MPesa kwa ajili ya malipo ya Rufaa (HESLB) imefutwa.Taratibu nyingine zinabaki palepale

Related Posts:

  • Zitto atuma waraka mzito kwa Mh. Lissu Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama – ACT Wazalendo , Zitto Kabwe amesema kuwa amefarijika sana kusikia sauti ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa hospitali Nairobi baada ya sauti yake kusikika jan… Read More
  • Gazeti la Tanzania Daima linaomba radhi   Kampuni ya Free Medea inayochapisha gazeti la Tanzania Daima, inaomba radhi kwa kuchapisha taarifa iliyokosewa. … Read More
  • Utafiti unaonesha Watanzania wanataka Katiba mpya   Utafiti wa Twaweza Tanzania unaonyesha kuwa asilimia 67 ya Watanzania wanasema ni muhimu kwa Tanzania kupata katiba mpya na asilimia 56 wanasema toleo la mwisho la rasimu ya katiba lipigiwe kura na wananchi. Ha… Read More
  • Mtoto wa Waziri Mkuu auawa kwa kisu   Mtoto wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania marehemu, Edward Moringe Sokoine, Kereto Sokoine ameauwa kwa kuchomwa kisu katika ugomvi ulitokea na mkewe hii leo mkoani Arusha. Kamanda wa Polisi mkoa wa … Read More
  • Tundu Lissu ameniagiza haya - Sugu   Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mh. Joseph Mbilinyi amefunguka na kusema ameagizwa na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kuwaambia wana Mbeya pamoja na Watan… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE