November 02, 2016

mashali-mazishi-22 

 mashali-mazishi-20

mashali-mazishi-9 
Rais wa TPBO, Yasin Abdallah ‘Ostadh’ akitoa heshima za mwisho.

mashali-mazishi-3 

HATIMAYE aliyekuwa bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali ‘Simba Asiyefugika’ leo amepumzishwa kwenye nyumba yake ya milele kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar akisindikizwa na mamia ya waombolezaji wakiwemo ndugu, jamaa na marafiki.
Mbali na hao, Mashali aliyeuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Jumatatu iliyopita huko Kimara-Bonyokwa, Dar, amesindikizwa kwenye safari yake hiyo ya mwisho na wanasoka, akiwemo Athuman Idd ‘Chuji’, mabondia maarufu Tanzania, Francis Cheka, Mada Maugo, Francis Miyeyusho, Japhet Kaseba na bondia mkongwe, Rashid Matumla.
Akizungumza na Global Digital kwenye msiba huo, Cheka alisema kuwa amesikitishwa sana na kifo cha Mashali ambaye kulikuwa na pambano kati yao lililokuwa linaandaliwa ambalo lilitarajiwa kufanyika Novemba 26, mwaka huu lakini hana budi kukubaliana na matokeo kwa sababu kila kitu kinapangwa na Mungu.
“Katika mapambano ya ngumi kwa upande wa uzito wa juu, kiukweli Tanzania imepoteza mtu muhimu sana. Mashali ameondoka wakati bado tasnia ya ngumi inamhitaji lakini ndiyo hivyo tena,” alisema Cheka.
Kwa upande wa meneja aliyefanya kazi kwa mara ya mwisho na Mashali, Sharifu Musili, alisema kuwa kifo cha Mashali kimetokea muda ambao hakuna aliyetarajia na kulikuwa na mipango mikubwa alikuwa anafanya juu ya bondia huyo.
“Tulikuwa tunafanya mipango Mashali akaishi nje ya nchi (Sweden au Ujerumani). Lakini kama haitoshi alikuwa na mapambano kadhaa ambayo alitakiwa kupambana. Moja lilikuwa tarehe 12, mwezi huu, lingine tarehe 26, mwezi huu na mengine mwezi unaofuata. Inasikitisha sana, nakosa hata maneno ya kuongeza,” alisema meneja huyo.
Mashali aliyeacha watoto saba, alizaliwa mwaka 1980, ameanza masuala ya ubondia mwanzoni mwa miaka ya 90 na hadi umauti unamkuta, alikuwa anamiliki mkanda wa dunia wa UBO.
Mikanda mingine aliyowahi kushinda ni ya Ubingwa wa WBF Afrika, Ubingwa wa IBF Afrika, Ubingwa wa TPBO Tanzania na Ubingwa wa PST Tanzania.
Marehemu Mashali au Simba Asiyefugika kwa upande wa viwango vya mabondia wa ngumi za kulipwa Tanzania, alikuwa ni wa pili huku nafasi ya kwanza ikishikiliwa na Cheka na ya tatu ikichukuliwa na Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’.

Stori/Picha: Boniphace Ngumije na Denis Mtima / GPL

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE