February 10, 2017


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hatokwenda polisi kwaajili ya mahojiano kama alivyoitwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akilitaja jina lake kwenye orodha ya pili ya watu wanaohusishwa na biashara ya dawa za kulevya.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Mbowe ambaye ni mbunge wa Hai na Kiongozi mkuu wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, amesema Makonda hana amri ya kumpa wito mtu kwenda polisi kwa mujibu wa sheria ya serikali za mitaa.
Amedai kuwa mkuu huyo wa mkoa ‘amenichafulia jina langu, chama, familia na upinzani.’ “Sijawahi kufanya biashara ama kutumia madawa ya kulevya wakati wowote katika maisha yangu,” amesema Mbowe.
“Mimi ni mtu mzima, ni kiongozi wa muda mrefu sijawahi kujihusisha kwa njia yoyote ama kuassociate na yeyote anayefanya biashara hiyo haramu ya madawa ya kulevya,” ameongeza.
Amedai kuwa licha ya kuunga mkono vita dhidi ya biashara ya madawa ya kulevya ambayo anaamini ilipaswa ianze zamani, lakini njia inayotumika ni ya hila na kinyume cha sheria.
                          

Related Posts:

  • Ally Nipishe - Wanapepeta Official Video Music Video Of Ally Nipishe under Visualization of AJ Production. The First Music Video After Sign A label contact with Papa Misifa , CEO Of MB Park'D Entertainment.      … Read More
  • Lowassa ampongeza kikwete   Lowassa na Kikwete  Waziri mkuu mstaafu na aliyekuwa mbunge wa monduli Mh: Edward lowassa ametoa salam nyingi za pongezi kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kwa utendaji wake wa kazi. Mh:Lowassa ameandika ayo… Read More
  • Majambazi yatikisa jiji la Dar es Salaam  Picha ya 1-2 ni mmoja wa watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi akiwa mikononi mwa polisi baada ya kutiwa mbaroni Mnara wa Saa maeneo ya Stesheni Dar es Salaam qleo mchana kwa madai ya kupora kiasi kikubwa cha fedh… Read More
  • New Audio/ Kura yangu - Mash j ft Vennt Skillz Mkali  wa Hip Hop toka mkoani Morogoro Mash J aliyetamba na wimbo kama Penny na Mperampera, hivi sasa amekuja na maamuzi sahihi juu ya Kura yake. Mash J ametoa maelekezo kwa viongizo wanaohitajika hasa kipindi hiki … Read More
  • Picha/ Mazishi ya mdau wa Media Frank Sanga wa Moro  Baba na mama wa marehemu Frank Sanga wakiweka shada  Mwakilishi wa Clouds media Daudi wa kota na mwakilishi wa wadau wa media Stanley Chinyuli wakiweka shada  Dada wa marehemu Frank, Esther Sanaga ak… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE