May 13, 2017

 

Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA na aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. Edward Lowassa amelaani vikali kitendo cha serikali ya Mkoa wa Dar es salam kuzuia kongamano la demokrasia lililopangwa kufanyika siku ya leo may 13, Mnazi mmoja jijini Dar es salaam. 
Mhe. Lowassa leo akizungumza na wanahabari ofisini kwake Mikocheni, Dar amesema kuwa amesikitishwa sana na serikali kuzuia kongamano ambalo lilikuwa na nia njema ya kuzungumza kuhusu demokrasia na kujifunza kutoka kwa watu mbali mbali jinsi ya kufanya siasa bila kukosea na kurekebishana penye makosa.
Mjumbe huyo ameendelea kufafanua kwamba hakuna tatizo kwa vyama vya siasa kutofautiana mawazo kwani ndiyo demokrasia na ndiyo sababu kubwa  ya waandaji kushirikisha watu wenye taaluma tofauti tofauti katika kongamano hilo.

 "Chadema kwa ujumla tunalaani sana kitendo cha Serikali ya Dar es salaam kuzuia mkutano wa amani wa kuwaunganisha watanzania pamoja kwa kutumia kongamano la demokrasia. Kitendo ambacho kimefanywa leo ni kuminya demokrasia. Nia ilikuwa njema na ndio maana waandaji wa kongamano waliweka picha yangu na kinana tukiwa tunatabasamu hivyo hakuna dhambi kwenye kutofautiana mawazo"- alisema Lowassa.
  

 Hata hivyo Mhe. Lowassa amekitaka chama cha Mapinduzi kutonyayasa upinzani kwa kuwa hawataweza kukaa madarakani muda wote huku akiwatahadharisha wakumbuke vyama vya ukombozi wa Afrika vilivyobaki madarakani ni  ANC na CCM.


Related Posts:

  • Hii ndiyo list ya walioingia tano bora tuzo za watu 2015 1-Video ya muziki inayopendwa  TZW13 Akadumba - Nay  Kipi Sijasikia – Prof J  Nani kama Mama – Bella  Wahalade - Barnaba  XO - Joh Makini  … Read More
  • Picha: Dayna Nyange katika muonekano huu mpya,   Pozi No.1  Mkali wa muziki wa bongo fleva Tanzania Dayna Nyange amekuja na muonekano huu mpya kwa sasa. Dayna ambaye anafanya poa sana na wimbo wake Nitulize aliomshirikisha Nay wa Mitego   Pozi … Read More
  • Jaguar awatibua mashabiki Marekani   Msanii wa kenya Jaguar Mwanamuziki wa Kenya Charles Njagua kanyi anayejulikana kama 'Jaguar' alitarajiwa kuwatumbuiza raia wa Atlanta nchini Marekani siku ya ijumaa lakini hakuonekana hadi asubuhi ya siku ya ju… Read More
  • Rwanda kuandaa CECAFA   Kocha mmoja wa Rwanda  Rwanda imeteuliwa kuwa mwenye wa fainali za kombe la mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFGA Challenge Cup, Novemba mwaka huu. Katibu mkuu wa CECAFA Nicholas… Read More
  • Msanii jela kwa kukejeli bendera ya Taifa   Msanii mmoja wa kucheza dansi , raia wa Armenia nchini Misri, amehukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani, kwa madai ya kutusi bendera ya taifa hilo. Msanii huyo anayefahamika kama Safinas, alihukumiwa kwa kosa l… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE