May 07, 2017

Picha ya baadhi ya wasichana wa Chibok waliotekwa nyara muda mfupi mwezi Mei 2014 
 Picha ya baadhi ya wasichana wa Chibok waliotekwa nyara muda mfupi mwezi Mei 2014

 Ofisi kuu ya Rais wa Nigeria imethibitisha kuwa wanafunzi 82 wa shule ya wasichana wa Chibok, waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram mnamo mwaka wa 2014, wameachiwa huru.
Maafisa wanasema kuwa waliachiwa huru, kufuatia majadiliano ya muda mrefu na ubadilishanaji washukiwa wa Boko Haram, waliokuwa wamezuiliwa na wakuu wa nchi hiyo.
Wasichana hao ni miongoni mwa zaidi ya wanafunzi wanafunzi 270 waliotekwa nyara kutoka shule ya malazi katika mji wa Chibok ulioko kaskazini mashariki mwa Nigeria.Wasichana hao wote 82 kwa sasa wanalindwa na jeshi la Nigeria mahali salama, baada ya kuletwa kwa barabara kutoka maeneo ya ndani kabisa vijijini, hadi katika kambi ya jeshi ya Banki, karibu na mpaka na Cameroon, hayo ni kwa mjibu wa mwaandishi habari wa BBC Stephanie Hegarty kutoka Lagos.

Wasichana 21 walioachiwa huru Oktoba 2016  
Wasichana 21 walioachiwa huru Oktoba 2016

Mwaandishi wetu anasema kuwa, familia nyingi huko Chibok wamefurahia taarifa hiyo ya hivi punde lakini wapiganaji hao wa Boko Haram, wangali wakiwazuilia zaidi ya wanafunzi 100.i sehemu ya maelfu ya watu ambao wametekwa nyara na wanamgambo hao, walioanzisha vuguvugu hilo miaka minane iliyopita.
Utekaji nyara huo ambao ulifahamika baadaye kama "Chibok girls" ulisababisha kilio kikubwa kote duniani na kampeini za kutaka waachiwe huru ikatanda kote katika mitandao ya kijamii.
Kabla ya hatua hii ya hivi punde ya kuwaachia wasichana hao, inakisiwa kuwa zaidi ya wasichana 195 wangali hawajulikani waliko.
Idadi ya washukiwa wa Boko Haram ambao wameachiwa huru na utawala wa Nigeria, bado haijajulikana.

Related Posts:

  • HAMIS MADOLE M/KITI MORO VETERAN APATA SHAHADA YA PILI   Madole ambaye kwa sasa ni Meneja NMB Mt. Uluguru Br.   WACHEZAJI wa klabu ya Morogoro Veteran wamempongeza Mwenyekiti wao, Hamis Madole (Mboma) kwa kuhitimu shahada ya pili ya corporate managenment (MBA) ka… Read More
  • MANDELA AWAPONZA DROGBA NA EBOUE  Wachezaji wa mpira wa miguu wa Ivory Coast, Didier Drogba na Emmanuel Eboue watawajibishwa na kamati ya nidhamu ya chama cha mpira wa miguu cha Uturuki, baada ya kuonesha uwanjani flana zenye maandis… Read More
  • DAYNA NYANGE: "TUSIMLILIE TU MANDELA"     Mwanamuziki wa Bongo Freva toka mkoani Morogoro Dayna Nyange ameandika ujumbe wake juu ya kifo cha mzee Nelson Mandela.     Katika AC yake ya Facebook Dayna ameandika Dayna nyange … Read More
  • PR. MUHONGO AWATOA JASHO MENGI, MNYIKA NA MTATIRO Jana nikikua katika mdahalo wa rasilimali pale ukumbi wa Nkurumah ,waliopewa nafasi ya kuzungumza katika kungamano lile ,Dr Mengi nea alipewa nafasi,yeye katika kuongea alikazia swala la watanzania wazawa wapewe nafasi … Read More
  • KANYE WEST AJIFANANISHA NA MANDELA Kanye West kwa mara nyingine tena anashambuliwa, hii ni mara baada ya hivi karibuni kusema kwamba muda si mrefu atakuwa ni mtu mkubwa kama nembo ya mtetea haki za binadamu zaidi ya Nelson Mandela.Kwenye mahojiano a… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE