September 30, 2017

Suala la Neymar bado ni bichi na inaonekana wazi kwamba Barcelona bado hawajaridhika na mchakato huo jinsi ulivyokwenda pamoja na ukweli kwamba tayari Neymar ameanza kuvaa jezi ya PSG.
Barcelona wameamua kurudi tena mahakamani kuishitaki PSG pamoja na wawakilishi wa Neymar kuhusu kiasi cha pesa ya ziada ambayo Barcelona waliitoa kwa wawakilishi wa Neymar wakati akienda PSG baada ya mchakato wa usajili kukamilika.
Gazeti moja maarufu la michezo nchini Hispania linasema kesi ya kwanza kati ya Barcelona na PSG ilimalizika na kila kitu kikaenda sawa lakini sasa Barcelona wameibuka upya na madai mengine kuhusu pesa hizo zaidi ya euro 26m.
Barcelona wanaamini kuna rushwa ilitembea kwenye upande mmoja wa usajili huku baba mzazi wa Neymar naye akihusishwa katika kesi hiyo ambapo Barcelona wanahitaji kiasi cha euro 8.6m kama fidia.
Baba mzazi wa Neymar na upande wa wawakilishi wa Neymar wanadaiwa walipokea zaidi ya euro 26m wakati wa mchakato wa usajili huo kitu ambacho kimewafanya Barcelona kuhisi kuna rushwa ilitendeka.
Tayari kesi hii imepelekwa mbele ya mahakama ya FIFA na pande zote tatu yaani Barcelona, baba mzazi wa Neymar ambaye ndio muwakilishi wake na PSG watakutana siku ya Jumanne kuanza kujadili kesi hii

Related Posts:

  • Kituo cha tembo yatima chafunguliwa   Srikali ya Tanzania imeanzisha kituo cha kwanza cha tembo yatima mjini Arusha. Kituo hicho kinatarajiwa kuhifadhi watoto wa tembo waliopoteza wazazi wao kutokana na vitendo vya ujangili au sababu nyengine. Hatua … Read More
  • Mbiyo za Urais ndani ya CCM, Mwigulu Nchemba achukua fomu leo      Mbio za kumpata mlithi wa kiti cha urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, zinazidi kushika kasi ndani ya chama cha mapinduzi-CCM baada ya wanachama kuzidi kuongezeka katika harakati za kumpata mgombe… Read More
  • January Makmba kufunguka jumapilu ijayo   Mbunge wa Bumbuli, Tanga na Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba nae ni mmoja wa walioingia kwenye headlines kwamba na yeye ameingia kwenye list ya wagombea wa CCM kwenye nafasi ya U… Read More
  • Waziri:Mbeki ndiye aliyetoa fedha kwa FIFA    Thabo Mbeki Waziri wa michezo wa Afrika Kusini , Fikile Mbalula, sasa anasema rais wa zamani wa Afrika kusini Thabo Mbeki ndie aliyeruhusu ulipwaji wa fedha ,dola milioni 10 kwa FIFA , hela ambayo sasa i… Read More
  • Mwasiti amshtua Babu Tale Ukimya wa msanii wa Bongo Fleva,Mwasiti Almas kwenye muziki umemshtua meneja wa msanii Diamond,Babu Tale. Babu Tale alimzungumzia msanii huyo hivi karibuni alipokuwa akifanya mahojiano kwenye kipindi cha XXL ambapo a… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE