Raila Odinga akiongea na waandishi wa habari mapema leo baada ya tamko la Mahakama
Maamuzi hayo ya mahakama yamekuja baada ya vyama vinavyounda umoja wa Upinzani (NASA), kupeleka malalamiko yao Mahakamani wakishutumu kudukuliwa kwa matokeo ya uchaguzi huo huku wakidai kuwa haukuwa wa huru na wa haki.
Hukumu hiyo imetolewa leo na jopo la majaji 6 na ilirushwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari nchini Kenya, imesema uchaguzi huo utarudiwa baada ya siku 60.
“Uchaguzi wa urais uliofanyika 8 Agosti, 2017, haukuandaliwa kwa mujibu wa katiba na sheria, hivyo matokeo yake ni batili. Natangaza kwamba Bw Kenyatta hakuchaguliwa na kutangazwa kwa njia inayofaa, agizo linatolewa na kuagiza Tume ya Uchaguzi kuandaa na kuitisha uchaguzi mwingine kwa kufuata katiba na sheria katika kipindi cha siku 60.“amesema Jaji Mkuu David Maraga.
Kiongozi wa upinzani, Raila Odinga amesema maamuzi hayo yaliyotolewa na Mahakama ni ya kihistoria na ni mfano wa kuigwa kwa nchi za bara la Afrika, huku akiondoa imani kwa tume ya taifa ya uchaguzi nchini humo IBEC.
“NASA hatuna imani tena na IEBC, na hakuna wa kuzuia safari yetu ya Kaanan, tunaishukuru mahakama kwa kutoa uamuzi huo,“amesema Raila Odinga.
Maamuzi hayo pia hayajawafurahisha viongozi wa upinzani pekee bali hadi kwa wafuasi wao kwenye miji mikubwa nchini humo kama Nairobi, Mombasa, Kisumu na miji mingine (Picha na BBC).
Wafuasi wa upinzani jijini Nairobi
0 MAONI YAKO:
Post a Comment