November 21, 2017


Aliyekuwa rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe.
SPIKA  wa bunge la Zimbabwe, Jacob Mudenda   jioni ya leo ametangaza kuwa rais Robert Mugabe amejiuzulu.
Spika huyo amesema kuwa hatua hiyo ni ya kujitolea na amefanya hivyo ili kuweza kuwepo kwa mabadiliko mazuri ya mamlaka kulingana na chombo cha habri cha reuters.
Tangazo hilo la ghafla lilizuia harakati za bunge kutaka kumng’oa madarakani ambazo zilikuwa zimeanza dhidi yake.
Wabunge walifurahia kufuatia hatua hiyo na raia wameanza kusherehekea barabarani.
Awali bwana Mugabe alikuwa amekataa kujiuzulu licha ya jeshi kuchukua mamlaka huku hatua hiyo ikifuatiwa na maadamano ya raia waliotaka kiongozi huyo kung’atuka mamlakani wiki hii.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE