November 07, 2017


 Mkurugenzi wa kundi la Unit Family  Deoglasi  Rusinde akizungumza kwenye ukumbi wa kituo cha Amani kilichopo Chamwino Morogoro

  Mkurugenzi wa kundi la Unit Family  Deoglasi  Rusinde akimkabidhi zawadi mbali mbali  Afisa Ustawi wa Jamii Kituo cha Amani Bw  SalvatoryAugustino[kulia]
 Baada ya kutoka Kituo ya Mehayo Mazimbu na baadae kituo cha Aman Chamwino kundi la Unit Family lilitia timu kituo cha Erick kilichopo Kiwanja cha Ndege eneo la Nanasi

 Ukibahatika kuingia mbinguni na usipomuona pepeponi Mama Josephini Bakhita unaweza kumhoji Mungu kwamba kwa nini Mama huyo hayupo Peponi kwa matendo mazuri aliyoyafanya duniani? Mama Makhita ambaye katika maisha yake alibahatika kupta mtoto tu Erick  Samanka mwenye ulemavu wa Viungo na akili. 
Akizungumza na Mtandao huu Mama Makhita alisema baada ya kumzaa mwanae akiwa na hali hiyo mwaka 1992 aliamua kuanzisha kituo cha Amani na kuwalea watoto wengine wenye matatizo kama ya Mwanae. 
" baada ya kuanzishi kituo hicho mwaka huu 92 nilipokea watoto wengi na kujikuta nikielemewa na majukumu ya kuwalisha na kuwatibu hivyo niliamua kukigawa kituo hicho kwa kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro
" Mwaka 2003 Mwanangu Erick aliaga dunia na mwaka 2009 nikiwa mtumishi wa serikali nilistaafu kazi na kujaliwa kujenga hii nyumba nikawiwa nikaamua kuanzishi kituo kingine hapa hapa nyumbani nilichokipa jina la Marehemu Mwangu Erick kwa sasa naishi na watoto 16 wenye matatizo mbali mbali''alisema mama huyo
 Mama alisema miongoni mwa watoto hao 16 yuko mtoto wa kimasai Joel  Yona[10] " Huyu mtoto alizaliwa akiwa na ulemavu wa akili na Viungo haqwezi kukaa wala kusimama mwingi analia maumivu. " Huyu baada ya kuzaliwa na hali hii wazazi wake walimtelekeza Mstuni kule Mvomero nikapata taarifa akapanda gari na kwenda kumchukua na kuishi naye hapa"alisema Mama huyo na kuongeza.
 " Kati ya walemavu  duniani kote walemavu hawa wenye ulemavu wa viungo na akili wanahitaji upendo na uangalizi wa karibu sana kwani ni tofauti na walemavu wengine ambao wanaweza kupambana na hali zao na kwenda nyumba za lbada au kwenye maduka mijini kuomba msaada tofauti na hawa ambao akili ya kutambua hilo hawana vile vile uwezo wa kutembea hawana"alisema mama huyo jambo lililoamsha vilio kutoka kwa watu waliokuwepo kanisani hapo pamoja na Askofu na mkewe

 Mama Makhita akitoka histori ya Mtoto huyo huku mtoto huyo akiangua kilia akilalamika maumivu, kitendo kilichowaliza wanafamilia wa kundi la Unit
 Wanachama wa Uniti wakiangua vilio

 Hebu cheki video ya tukio hilo
 Mtoto Joel akishushwa kwenye kifaa chake cha kisimamia
 Watoto Joel[10] Kulia na Grece Emmanuel[17] wakiwa na walezi wao. licha ya umri mkubwa Grece anaonekana kuwa an sawa na Joel kufuatia kusumbuliwa na maradhi.
 Mkurugenzi wa Uniti family Deoglas  Rusinde[kulia kwa kushirikiana na Katibu wa kanisa la EAGT Sayuni Temple Bw Whery Lyimo Wakimkabidhi zawadi Mama Makhita
 Kundi la Uniti Falmily wakipiga Picha ya pamoja na watoto wa kituo cha Erick
 .... Baada ya kukabidhi zawadi hilo wana Unit Family waliangusha maombi kwa watoto hao
 .....Mwandishi wa Mtandao huu mwenye flana ya mistari akishiriki kuangusha maombi kwa watoto hao
 Baada ya maombi kukalea Mtoto huyu alipandwa na mapepo


  Baada ya kutoka Kituo cha Erick Mwandishi wa Mtandao huu alitinga ofisni kwa Askofu wa Kanisa la EAGT Satubi Tenple  Askofu Peter Denis na kufanya naye mahojiano ofisini kwake
 Kanisa la EAGT Sayi=uni Temple lililopo Pande za Chwamino Morogoro

 

 Mkurugenzi wa Unit Family ]kati] akizungumza ofisni kwa Askofu Densi kabla ya Tamasha hilo kuanza[ kushoto na Mgeni rasm Bw Fiume na kulia ni Askofu Denis

 

 ...Watoto hao walila chakula ndani ya kanisa hilo

Mama Makhita akifika kanisani hapo na mwane Joel





 Waasisi wa Vituo vya kulelea watoto wenye matatizo mbali mbali Josephini Bakhita[kushoto] kituo cha Aman na Rinda  Ng'ido wa kituo cha Mehayo Mazimbu
 Mama Rinda akizungumza
 Mama Bakhita akizungumza kanisani hapo
 Askofu Denisi aliamulu kanisa lote kiweka mikoto juu ya watoto hao wakati akiwafanya maombi
 Watoto Joel kushoto na Grece kulia wakipokea maombi kutoka kwa Askofu
 Maneno yaliyokuwa yakitamkwa kwenye maombi hayo yaliwaliza wengi kanisani hapo ambapo Mwandishi wa Mtandao huu pia alishindwa kuzuia chozi lake na kumwagika



  Mke wa Askofu Denis Bi, Mwamini Denisi naye akimwaga chozi wakati mumewe akiwaombe watoto hao
 ...Baada ya Maombi na kushuhudia sehemu kubwa ya kanisa wakiangua vilio Askofu Denis alijikuta naye akitokwa na chozi
 MUNGU ni mwema baada ya maombi hayo mazito maumivu ya Mtoto Joel yalipungua kama alivyonasw ana kamera ya mtandao huu kanisani hapo
 Baada ya maombi viongozi hao walikata keki na kula na watoto hao
 ......Wakiikata keki

 ....Mgeni rasm akimrisha mmoja wawato hao
 ...Askofu akimrisha keki mgeni rasm
 Mama Askofu akimrisha keki mumewe
 Bingwa wa salam redio Tanzania Matata Ndizi ambaye ni mwanachama Pekee wa kundi la Unit Family kutoka nje ya Dar akihojiwa na Mtandao huu. lfahamike Matata Ndizi ni mfanyabiashara wa Soko Mkuu Morogoro
 Kiongozi wa kundi la Unit Family akimkabidhi baiskel 2 mgeni rasm ambaue naye alikabidhi zawadi hizi kwa mmiliki wa kituo cha Mehayo Mama Rinda






Stori: Dunstan Shekidele,Morogoro
Mtoto wa kimasai aliyetupwa na wazazi wake baada ya kuzaliwa akiwa na ulemavu wa viungo na akili , Joel Yona (10) ambaye hawezi kukaa wala kusimama, amewaliza wengi akiwemo Askofu Peter Denis wa Kanisa la EAGT Sayuni Temple lililipo Chamwino mjini hapa.

Wiki iliyopita, katika kuadhimisha miaka 7 tangu kuanzishwa kwa kikundi cha Unit Family kutoka jijini Dar, kinachojihusisha na utoaji misaada kwa watu wenye mahitaji maalum, kiliamua kufika Mkoani hapa kutembelea vituo vya watoto mbalimbali.
Miongoni mwa vituo walivyotembelea ni kituo cha Mehayo kilichopo Mazimbu, Aman kilichopo Chamwino na Erick kilichopo kiwanja cha Ndege ambapo Unit Familly waliwaalika watoto wote wa Vituo hivyo kwenye tamasha lilifanyika kanisani hapo.

Katika Tamasha hili ambalo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dr. Kebwe Stephen Kebwe aliyewakilishwa na Afisa Biashara wa Manispaa ya Morogoro, Mfaume Fiume, wanachama zaidi ya 20 wa Unit Familly walikula na kunywa na watoto hao na baadae kukabidhi zawadi kwa watoto zikiwemo baiskeli mbili za matairi.

Awali, Unit Familly waliguswa zaidi na kujikuta wakiangua vilio baada ya kutembelea kituo hicho cha Erick na kuguswa na ugonjwa na historia ya mtoto Joel,.

Aidha, mbali na maradhi na historia ya Joel pia waliguswa na mwezake Grace Emmanuel (17) ambaye naye historia ya maisha yake illitolewa kanisani hapo na mlezi wao Josephine Bakhita.

Akizungumza kwenye tamasha hilo, Askofu Denis alisema: "Naamini Mungu anaweza kuwaponya watoto hawa hata sasa hivi, lakini ana kusudi maalum la kuwaacha kuwa walivyo".

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Fiume alisema: "Serikali ya Mkoa wa Morogoro inatambua uwepo wa vituo hivyo vitatu na kupitia tamasha hili tutaongeza juhudi za kuvihudumia vituo hivyo"
Kwa upande wake mkurugenzi wa Unit Family Deoglas Rusinde ambaye pia ni Produse wa kipindi cha Njia Pande Radio Clouds alisema.
” Kundi letu la Unit Family linalojihusisha na utaoaji misaada kwa watu wenye uhitaji maalumu kwa wanakikundi kujichangisha limetimiza miaka 7 toka kuanzishwa hivyo tumeona Mwaka huu tuje morogoro kujumuika na watu wenye matatizo mbali mbali”alisema Mkurugenzi huyo

Katika Tamasha hilo waimbaji Maarufu wa ijiniri kutoka Dar na Moro walipafomu akiwemo dereva Maarufu wa SUA Mzee Tegemea Leonald.
  Picha za waimbaji hao zitawajia hivi punde endelea kuwa jirani na Mtandao huu muda wote.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE