February 16, 2018

Mwenyekiti wa Chaumma, Hashim Rungwe Spunda ameungana na Chadema kumnadi mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni, Salumu Mwalimu na kuwaomba wananchi wampigie kula akidai kuwa mgombea wa CCM ni msaliti na hawapaswi kumchagua.

Rungwe ameilaumu Serikali ya awamu hii kufanya kazi zao kwa kuwatumia polisi kukamata watu na kuwaweka ndani.

”Tumeona tawala nyingi lakini mmeshawahi kuona utawala wa namna hii? Yaani polisi ndiyo wanafanya serikali ifanye kazi yaani bila ya polisi hawafanyi kazi, polisi ndiyo wamewekwa mbele yaani ukisema hivi unakamatwa” Amesema Rungwe.

Rungwe aliendelea kuelezea juu ya sakata lake la kukamatwa na polisi siku za karibuni.

“Mnakumbuka mimi nilikamatwa juzi juzi hapa yaani hakuna kitu chochote cha maana mpaka sasa mimi ni Wakili na Wakili kazi yake ni kusaini nyaraka, nimesaini nyaraka za watu na hao watu wenye pesa walikuwa wakitoa maagizo mlipe huyu na huyu na mimi nalipa sasa mimi nimefanya kosa gani? Hawa watu ni wabaya na haya ni mambo ya serikali ya CCM, hakikisheni kwamba serikali ya CCM mnaiondoa msikubali Mtulia awe Mbunge wenu. CCM ndiye wanaiharibu nchi hii” alisisitiza Rungwe.

Aidha ameongezea kuwa, “Serikali hii ya CCM inajidai sanaa inafanya propaganda kwenye Radio na kila mahali lakini mimi naomba niulize wangapi wamekuja hapa hawana kitu mfukoni, mna hela nyie? Wananchi hali zao mbaya watu hawana kitu.

Hivyo amewaomba wananchi kumchagua kiongozi kutokana na mambo anayoyafanya na kuwasisitizia wasimchague mgombea huyo toka chama cha CCM.

Related Posts:

  • PAPA AWASILI UFILIPINO Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani,Mtakatifu Francis, amewasili nchini Ufilipino, nchi yenye Wakatoliki wengi zaidi barani Asia, huku ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa. Maelfu ya Wafilipino wamejipanga katika misur… Read More
  • NEW VIDEO: KIBOKO YANGU- MWANA FA ft ALLY KIBA Hii ni video mpya ya mkali Hamisi Corleone Mwinjuma aka Mwana FA ya Kiboko yangu ni moja kati ya ambazo zimekuwa zikisubiriwa kwa hamu na watu wengi. Video imetayarishwa na Director Kelvin Bosco wa … Read More
  • RONALDO DE LIMA KUREJEA DIMBANI Ronaldo de Lima anavyoonekana sasa. Mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya brazil Ronaldo Luís Nazário de Lima anatarajia kurejea tena dimbani. De lima ameahidi kupunguza… Read More
  • MARKEL: TUTAWALINDA WAYAHUDI NA WAISLA,U UJERUMANI Kansela Angela Merkel   Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel ameahidi kuwalinda Wayahudi na Waislamu wanaoishi nchini Ujerumani dhidi ya ubaguzi. Amesema demokrasia ndiyo njia bora ya kupambana na machafuko yanayo… Read More
  • WATANZANIA WENGI WAFUNGWA HONG KONG Kasisi mmoja raia wa Australia amefichua na kuthibitisha kuwa kuna idadi kubwa ya wafungwa wenye asili ya Afrika katika magereza ya Hong Kong, wengi wao wakiwa ni kutoka Tanzania. Kasisi huyo John Wortherspoon ambaye … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE