May 08, 2014


  Baada ya tuzo za KTMA kumalizika kila mmoja amekuwa na mtazamo wake, wiki hii producer wa wimbo wa ‘Number One’ wa Diamond, Sheddy Clever alitoa malalamiko yake ya kukosa tuzo ya mtayarishaji bora huku wimbo alioutengeneza ukimpa Diamond zaidi ya tuzo tano.
Producer mkongwe Joachim Kimaryo aka Master J ametoa mtazamo wake kuhusu tuzo za KTMA 2014 ambao unaonesha hakuridhishwa na mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa mwaka – kizazi kipya ambaye ni Man Water wa Combinenga.
“Sijaelewa damond kupata tuzo 7 alafu produza wake kutoka na 0!!!!!” ni jibu la moja ya maswali kuhusiana na tuzo hizo aliyokutana nayo Master J Jana alipokuwa mgeni katika session ya ‘Kikaangoni Live’ kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV.
Shabiki mwingine aliuliza: “Pia man water ni mkali au unasemaje master J?”
Na hiki ndicho alichojibu Jay: “mkali lakini hakusahili kushinda mwaka huu”

Swali tofauti na muziki ambalo lilijirudia mara nyingi ni kuhusu uhusiano wake na mpenzi wake Shaa, shabiki mmoja aliuliza:
“Mnafunga ndoa lini ww na Shaa manake mnapendezana kweli? Au ni mchepuko tu wa lami?

Na jibu la Joachim aka Master J mabibi na mabwana lilikuwa “SOON”.

Related Posts:

  • B Dozen atia neno mvutano wa Diamond na Alikiba Mtangazaji wa kipindi cha XXL cha Clouds Fm,Hamis Burhani Mandi B Dozen amefunguka mambo machache kuhusu mvutano wa Diamond na Alikiba pamoja na team zao katika mitandao ya kijamii. Katika mahojiano na Times Fm kweny… Read More
  • Official Music Video: Muda - Chidi Beenz feat. Q Chief   Chidi Benzi Chuma, ametuletea Video ya wimbo wake wa Muda aliomshirikisha Q-Chief. Story zinazidi kusambaa mitandaoni na kwenye vyombo mbalimbali vya habari, je ametengeneza kiki ili aachie Video?? Jibu unalo wewe … Read More
  • Mtoto wa Shilole kugundua dawa ya UKIMWI Shilole msanii wa muziki na filamu wa Tanzania.    Msanii Shilole ameweka wazi kile ambacho watu wengi walikuwa hawafahamu kuhusu watoto wake, na kusema kwamba mambo yake ya mitandaoni hayawaathiri … Read More
  • Official HD Video :Nisamehe Bure -Ochusheggy   Ukali, uwezo na ubora wa sauti yake, tunaweza sema vya kulithi siku zote huwa vinazidi. Ochu Sheddy mtoto wa mwanamuziki mkongwe nchini Eddy Sheggy, ametuletea wimbo wake mpya u naitwa Nisamehe Bure   &… Read More
  • Hakuna mwenye pesa - Alikiba Allikiba Mkali wa 'Seduce Me'  Ally Salehe Kiba, amefunguka na kusema katu hataweza kuishi maisha ya kuigiza umaarufu kwani anaamini watu ndiyo waliompokea kipindi akiwa han… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE