May 08, 2014


  Baada ya tuzo za KTMA kumalizika kila mmoja amekuwa na mtazamo wake, wiki hii producer wa wimbo wa ‘Number One’ wa Diamond, Sheddy Clever alitoa malalamiko yake ya kukosa tuzo ya mtayarishaji bora huku wimbo alioutengeneza ukimpa Diamond zaidi ya tuzo tano.
Producer mkongwe Joachim Kimaryo aka Master J ametoa mtazamo wake kuhusu tuzo za KTMA 2014 ambao unaonesha hakuridhishwa na mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa mwaka – kizazi kipya ambaye ni Man Water wa Combinenga.
“Sijaelewa damond kupata tuzo 7 alafu produza wake kutoka na 0!!!!!” ni jibu la moja ya maswali kuhusiana na tuzo hizo aliyokutana nayo Master J Jana alipokuwa mgeni katika session ya ‘Kikaangoni Live’ kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV.
Shabiki mwingine aliuliza: “Pia man water ni mkali au unasemaje master J?”
Na hiki ndicho alichojibu Jay: “mkali lakini hakusahili kushinda mwaka huu”

Swali tofauti na muziki ambalo lilijirudia mara nyingi ni kuhusu uhusiano wake na mpenzi wake Shaa, shabiki mmoja aliuliza:
“Mnafunga ndoa lini ww na Shaa manake mnapendezana kweli? Au ni mchepuko tu wa lami?

Na jibu la Joachim aka Master J mabibi na mabwana lilikuwa “SOON”.

Related Posts:

  • Matumla afanya kweli Mohamed Matumla akijitahidi kumbana vyema mpinzani wake Bondia Mohamed Matumla amefanikiwa kutoka kimasomaso baada ya kumchapa kwa points bondia mwenzake kutoka nchini China Wang Xin Hua katika mpambano wa raundi 10 uli… Read More
  • Mtoto wa miaka 2 avunja rekodi Mtoto wa miaka 2 aweka rekodi India Amini usiamini mtoto mwenye umri wa miaka miwili ameweka rekodi ya taifa ya ulengaji shabaha kwa mishale nchini India.  Kulingana na vitabu vya kumbukumbu ya rekodi za taifa, Dolly S… Read More
  • Kuhusu ajali ya ndege iliyopindika, kumbe Rubani alikuwa na matatizo ya kiakiliAjali ya ndege Viongozi wa mashtaka nchini Ujerumani wanasema kuwa wamepata ushahidi unaosema kwamba rubani wa ndege ya Ujerumani ilioanguka katika milima ya ALPS na kuwaua abiria 150 alikuwa amemficha mwajiri wake kuhusu ugo… Read More
  • Muswada tata kupeleka waandishi jela wapita Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bunge limepitisha muswada mchungu kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari baada ya kupitisha Muswada wa Takwimu wa Mwaka 2013, ambao pamoja na mambo mengine unataka mwandishi at… Read More
  • Kampuni ya Fantastic & Cool Object yapania kuleta mabadiliko  Baadhi ya wasanii waliopo chini ya Fantastic  Kampuni mpya ya Fantastic & Cool Object ya nchini Tanzania, imedhamilia kuleta mabadiliko kwa watanzania kwa kuanzia na wasanii wa Bongo Fleva.  Mkur… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE