November 14, 2014


 
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Jacqueline Wolper. 
Chanzo makini kilichopo ndani ya kamati ya wasanii hao wa Bongo Movies, kitendo cha Taasisi ya Twaweza kutangaza kuwa Lowassa anaongoza na kuwagaragaza makada wenzake ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwao ni ishara tosha ya ushindi wa kishindo katika uchaguzi ujao. 
SIKU chache baada ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kutangazwa kuwa anaongoza katika kinyang’anyiro cha urais 2015, mastaa mbalimbali wanaomuunga mkono wameandaa mkakati wa kumfanyia sherehe ya kumpongeza. 
“Mastaa wa Bongo Movies wanaomuunga mkono Lowassa wameandaa bonge la pati la kumpongeza Lowassa na siku hiyo watakula, watakunywa maana mipango yao tayari wanaona inakwenda vizuri na hakuna mtu ambaye anaweza kumuangusha katika chama hicho,” kilisema chanzo bila kutaja lini na wapi watakapofanyia sherehe hiyo. 
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Esha Buheti. 
Mbali na sherehe hiyo kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali, chanzo hicho kimeeleza kuwa wanatarajiwa pia kualikwa wananchi mbalimbali wanaomuunga mkono Lowassa. 

“Safari ya kuelekea uchaguzi mkuu ndiyo imeanza rasmi, Twaweza wametafiti na kubaini kile ambacho sisi tulikuwa tunakiamini, Lowassa hana mpinzani CCM, ushindi ni lazima,” kilisema chanzo hicho. 
 
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Mahsein Awadhi.
 Wasanii ambao wanatajwa kuwa upande wa Lowassa ni Jacqueline Wolper, Esha Buheti, Mahsein Awadhi ‘Dk. Cheni’, Wema Sepetu ‘Madam’ na wengine kibao. Taasisi ya Twaweza iliyofanya utafiti kwa mwezi Septemba, ilitangaza matokeo hayo Jumatano iliyopita na mtafiti wake, Elvis Mushi ambapo alisema wananchi 1,445 walihojiwa kwa njia ya simu ambapo Lowassa alipata asilimia 13 huku waziri mkuu wa sasa, Mizengo Pinda akimfuatia kwa kupata asilimia 12. 
 
Wema Sepetu ‘Madam.
 Wengine waliopigiwa kura katika utafiti huo ni Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbrod Slaa aliyepata asilimia 11, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akipata asilimia 6 huku Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe akiondoka na asilimia 5.

Related Posts:

  • Usafiri wa Mwendokasi umesitishwa   Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 11:00 alfajiri kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la … Read More
  • Yanga yaenda Ethiopia bila nyota wake Klabu ya soka ya Yanga imesafiri kuelekea nchini Ethiopia leo Alfajiri ikiwa na kikosi cha wachezaji 20 na viongozi 13 wakiwemo 8 wa benchi la ufundi. Lakini timu hiyo imesafiri bila ya nyota wake Ibrahim Ajib amba… Read More
  • Official video: Bora Nife - Aslay X Bahati Mwanamuziki Aslay kutoka nchini tanzania, amevuka mipaka mpaka kufikia code ya +254 namaanisha nchi jirani ya Kenya na kukutana na mwanamuziki Bahati na kufanya huu wimbo wa Bora Nife.      … Read More
  • Uchaguzi TLS, Wakili Fatma Karume amlithi Tundu Lissu   Wakili Msomi Fatma Karume ameshinda nafasi ya Urais wa Chama Cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) na kuwa mrithi wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambaye amemaliza muda wake leo kutumikia nafasi hiyo kama R… Read More
  • Monalisa aibuka muigizaji bora Afrika   Mona akiwa na mpinzani wake Lupita Nyongo toka Kenya   Mrembo na muigizaji mkongwe kwenye tasnia ya filamu nchini Yvonne Cherrie maarufu kama 'Monalisa'  ameibuka mshindi kwenye tuzo za 'The African P… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE