January 19, 2015

Mohammad Javad Zarif  
Mohammad Javad Zarif
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali mauaji ya wanachama sita wa Harakati ya Mapambano ya Lebanon Hizbullah yaliyofanywa na utawala haramu wa Kizayuni. Akizungumza na televisheni ya Press mapema leo, Muhammad Javad Zarif Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Tehran inalaani vikali vitendo vyote vya kigaidi vya utawala wa Kizayuni wa Israel  vikiwemo vile vinavyotekelezwa na utawala huo dhidi ya watu wa Lebanon na Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya nchi hiyo. Zarif amesema sera ya ugaidi wa kiserikali ni sera inayofahamika ya utawala wa Kizayuni wa Israel. Harakati ya Mapambano ya Lebanon Hizbullah imethibitisha kuuliwa wapiganaji wake sita katika shambulio jipya la anga lililofanywa na Israel katika mji wa kistratejia wa Quneira kusini magharibi mwa Syria. Hizbullah imewataja wanachama wake waliouliwa jana na Israel kuwa ni Jihad Mughniya mwana wa kiume wa Imad Mughniya kamanda wa ngazi ya juu wa harakati hiyo aliyeuliwa kigaidi na Israel na wapiganaji wengine watano waliotajwa kwa majina ya Mohammad Issa aliyekuwa na miaka 42, Abbas Ibrahim Hijazi miaka 35, Mohammad Ali Hasan Abu al Hassan miaka 29, Ghazi Ali Dawi miaka 26 na Ali Hasan Ibrahim miaka 21.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE