January 19, 2015

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/5e392c4d9cc51aa660a90bec0219f5d3_XL.jpg 
 Wanamapinduzi wa Kishia wa Ansarullah wa nchini Yemen wamepigana na vikosi vya serikali huko Sana'a mji mkuu wa nchi hiyo. Watu walioshuhudia wamesema kuwa, sauti za risasi na milipuko kadhaa zimesikika huko Sana'a na karibu na ikulu ya Rais kusini mwa mji mkuu huo. Maafisa usalama wa Yemen walifunga barabara zinazoelekea katika ikulu ya rais, huku ripoti nyingine zikisema kuwa mapigano yamejiri ndani ya ikulu hiyo, huku moshi ukishuhudiwa katika eneo hilo.
Wakati huo huo kanali ya televisheni ya wapiganaji wa Kihouthi imetangaza kuwa vikosi vya jeshi la Yemen vilifyatua risasi wakati vikipiga doria katika ikulu ya rais, hatua iliyosababisha ghasia. Mivutano imekuwa ikishadidi huko Yemen kati ya wapiganaji wa Ansarullah wanaojulikana pia kwa jina la Mahouthi na vikosi vya serikali, baada ya wapiganaji hao wa Kishia kumtia mbaroni Ahmed Awad bin Mubarak, mkurugenzi wa ofisi ya Rais Abdrabuh Mansour Hadi wa Yemen. Mubarak alitiwa nguvuni katika kituo kimoja cha upekuzi katika mkoa wa Hada kusini mwa Yemen.

Related Posts:

  • Kutana na mashairi ya siachani nawe ya Baraka da Prince (verse1) Wakati nalainisha moyo kupenda sio kama ninakosea ipo sababu ya mimi kurejesha namba ambayo ilipotea hali ya mtoto kumsusa mama akishachapwa ni sawa na mapenzi ukishapendwa unasahau hata kama ulishafanyiw… Read More
  • Aunt Ezekiel ajifungua mtoto wa kike   Na Andrew Chale, Modewji blog Ilikuwa si rahisi kama ilivyojulikana na wengi hasa kwa namna ya ‘fans’ wa staa wa filamu za Bongo maalufu  Bongo  Movie,  kujua  hatma ya ujauzito wake ambao u… Read More
  • Mtu mmoja apigwa risasi    Habari kutoka Burundi zinasema kuwa mtu mmoja amepigwa risasi na kuuawa katika mji mkuu wa Bujumbura. Mtu huyo alikuwa miongoni mwa waandamanaji wanaopinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza kugombea urais kwa aw… Read More
  • Sterling apata mtetezi   Nyota wa Liverpool Raheem Sterling ametetewa kwa kuwa na hamu kujiunga na vilabu vikubwa. Mshambuliaji huyo wa Liverpool huenda asilaumiwe kwa kuonyesha hamu ya kung'aa zaidi na kutaka kushinda vikombe. Hii ni kw… Read More
  • Rais Jacob Zuma awaomba radhi raia wa Msumbiji Hatimaye Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amewaomba radhi raia wa Msumbiji. Rais Zuma amechukua hatua hiyo kufuatia kuuliwa raia kadhaa wa Msumbiji, katika vurugu zilizoambatana na mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni n… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE