January 10, 2015


 Star wa muziki Ali Kiba, amesema kuwa mapokezi ya video yake ya Mwana ndani na nje ya mipaka ya Tanzania yamekuwa ni ishara kwake kuwa kuna mtu alikuwa amemiss katika game na katika mchango wa kuitangaza nchi kimataifa kupitia sanaa.
Kiba a.k.a Fundi ameiambia eNewz kuwa amefurahi kuona mashabiki wamempokea tena vizuri na kumpa nguvu ya kuendelea kuwatengenezea kazi zenye viwango vya kimataifa.
Kuhusiana na kiu ya mashabiki wengi kujua Kiba mwaka huu ana uanzaje, na vilevile kuhusiana na kolabo za kimataifa, Kiba amesema mipango imeshasukwa, akiwa amejipanga kutoa kazi kwa mtindo wa Bumper 2 Bumper, mpango utakaoanza mwezi huu wa Januari.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE