January 24, 2015

Tangazo la mfalme mpya wa Saudi Arabia, Salman, Januari 23 mwaka 2015 mjini Riyad. 
 Salman bin Abdulaziz al-Saud, ndugu wa Abdullah na mtoto wa mwanzilishi wa ufalme, hatimaye ni mfalme wa Saudi Arabia na mlinzi wa maeneo mawili takatifu ya Uislamu.

 Ijumaa, Januari 23, baada ya kutangazwa kifo cha Abdullah, mfalme Salman aliitisha mara moja kikao cha Baraza la utawala wa kifalme na kuteuliwa ndugu yake mwingine, Moqren, kama mrithi wake.
Wakati huo huo mfalme Salman ameongea kwenye televisheni ya taifa akihakikishia ulimwengu na raia wa Saudia mwendelezo wa utawala wa kifalme na sera zake.
Katika hotuba yake ya kwanza ya mfalme, Salman wa Saudi Arabia, mwenye umri wa miaka 79, amethibitisha kwamba hakutakuwa na mabadiliko katika siasa za nchi.
" Sisi tutakaa na nguvu ya Mungu, kwenye njia ya haki ambayo taifa hili lilifuata tangu kuanzishwa kwake na mfalme Abdul Aziz bin Saud na wanawe baada yake", amesema mfalme Salman.
" Mungu alitaka mimi nipewe majukumu haya makubwa, naomba kwa Mungu anipe msaada huo", ameongeza mfalme Salman.
Saudi Arabia ni nchi ya kwanza kwa uzalishaji wa mafuta. Uzalishaji wake wa dhahabu nyeusi unalinda ushawishi wa shirikisho la la nchi zinazouza mafuta (Opep). Saudi Arabia pia ni mchangiaji muhimu katika mahusiano na Mashariki ya Kati, hasa katika miaka ya hivi karibuni. Riyadh ni mshirika muhimu wa Marekani na nchi za Magharibi katika sekta ya kidiplomasia.
Serikali ya Saudi Arabia ina mwelekeo wa Kiislamu. Mfalme mpya ametoa wito kwa umoja miongoni mwa Waislamu ambao wamegawanyika kutokana na vita vinavuendelea duniani.

Related Posts:

  • Diamond avunja rekodi Trace TV Kwenye Top 10 ya muziki mkali wa Afrika ambayo hufanyika kila Alhamisi kwenye kituo cha TV cha Ufaransa ambacho kina mamilioni ya Watazamaji Afrika (TRACE TV Urban) July 2, 2015 single ya ‘Nana’ Diamond ft Mr Flavour … Read More
  • Dayna Nyange aomba jamii Dayna Nyange akiwa na Ney wa Mitego Mwanadada anayekuja kwa kasi katika muziki wa bongo, Dayna Nyange, ameiomba jamii isimfikirie vibaya kuhusu wimbo wake wa Nitulize. Kauli ya msanii huyo imekuja baad… Read More
  • New audio/ Edina- Best Nasso Hii ningoma mpya kabisa kutoka kwa mkali wa nyimbo za hisia Best Nasso, hapa kamuimbia Edina … Read More
  • Rais Kikwete aongoza mazishi ya Chifu Kingalui 14 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole na pia kumpongeza Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru wa Mkoa wa Morogoro Chifu Kingalu wa 15  baada ya kusimikwa rasmi kijijini Kinole mkoani Morogoro jana Alhamis… Read More
  • Kikwete ashuhudia kusimikwa kwa Kingalu mwana Banzi wa 15 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia kusimikwa kwa Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 katika kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 2, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE