January 26, 2015

Armel Mingatoloum Sayo, Waziri wa Vijana, Michezo, Sanaa na Utamaduni wa CAR aliyetekwa nyara na magaidi wa Anti-Balaka 
 Armel Mingatoloum Sayo, Waziri wa Vijana, Michezo, Sanaa na Utamaduni wa CAR aliyetekwa nyara na magaidi wa Anti-Balaka
 Watu wanaosadikiwa kuwa wanamgambo wa kundi la kigaidi la Anti-Balaka la Jamhuri ya Afrika ya Kati wamemtaka nyara Waziri wa Vijana, Michezo, Sanaa na Utamaduni wa nchi hiyo. Nicaise Danielle Sayo mke wa waziri aliyetekwa nyara na magaidi wa Anti-Balaka amesema kwamba, tukio hilo lilitokea wakati yeye na mumewe walipokuwa wakirejea nyumbani wakitokea kanisani, ambapo watu wasiojulikana walipomteka nyara mumewe katika eneo la Galabadja jirani na mji mkuu Bangui. Taarifa zaidi zinasema, baada ya Anti-Balaka kumteka nyara Armel Mingatoloum Sayo, Waziri wa Vijana, Michezo, Sanaa na Utamaduni walimtia katika gari na kuondoka naye kuelekea katika ngome yao huko Boy-Rabe. Mashirika ya kutetea haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa yametahadharisha kuhusiana na kuongezeka jinai za kivita katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
 Waziri huyo ametekwa nyara siku moja tu baada ya Rais Bi. Catherine Samba-Panza wa nchi hiyo kulaani vikali vitendo vya kutekwa nyara watu nchini humo kunakofanywa na watu waaobeba silaha. Hayo yanajiri katika hali ambayo, Jamhuri ya Afrika ya Kati imeendelea kushuhudia machafuko na hivyo kuzorotesha shughuli pamoja na maisha ya kawaida ya wananchi wa nchi hiyo. Jamhuri ya Afrika ya Kati ilitumbukia kwenye machafuko na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe baada ya kuondolewa madarakani serikali ya Rais Francois Bozize, mapigano ambayo hadi sasa yamepelekea Waislamu wengi kuuawa. Kundi la kigaidi la Kikristo la Anti-Balaka limekuwa likiwalenga kwa makusudi Waislamu wa nchi hiyo katika mashambulio yao. Maelfu ya Waislamu wa nchi hiyo wamelazimika kuyakimbia makazi yao wakihofia usalama wa maisha yao.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE