Askofu
wa kanisa kathoriki jimbo la morogoro Askofu Christopher Mkude ameonya kauli ya ccmya kushinda
hata kwa goli la mkono na ile ya UKAWA inayowataka wafuasi wao kulinda
kura ktk uchaguzi mkuu ni kauli za kichochezi zinaweza kuchochea
uvunjifu wa amani ya nchi. Mkude alikuwa akizungumza na waandishi wa
habari ofisini kwake ambao walikwenda kuutambulisha uongozi mpya wa
chama cha waandishi wa habari mkoa wa Morogoro (Moro
press) uongozi uliopo chini ya uenyekiti wa Nickson Mkilanya.
"Tutashinda hata Kwa goli la mkono maana yake nini? Kwamba watashind
Kwa njia yoyote Ile hata ya kuiba au maana yake nini? lakini kibaya
zaidi kauli hiyo haijawahi kukemewa hata na wakubwa wake"alisema askof Mkude na kuongea Hawa wengine wanasema walinde kura kwani Hawana
mawakala pale? wanataka kusema kuwa ni lazima washinde wao na jee
wasiposhinda ?hizi ni kauli mbaya ambazo watanzania kwa imani zetu zote
hatupaswi kuzifuata. Nchi hii yetu sote wakristo, waislam na hata wasio
na dini na wasio wanasiasa tulinde amani yetu uchaguzi uishe kwa amani
na kila mmoja asiwe chanzo cha kuharibu amani yetu. Uchaguzi mkuu
utafanyika nchini kote siku ya Tarehe 25 jumapili ijayo
Prof Kitila: Tunahitaji vyombo vya habari imara
-
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwezeshaji, Profesa Kitila
Mkumbo, amesema Serikali...
6 hours ago
0 MAONI YAKO:
Post a Comment