
Uzinduzi huo umefanyika kwenye kiwanda
hicho kipya kilichopo eneo la Msijute, Mtwara Vijijini mkoa wa Mtwara na
kuhudhuriwa na wafanyabiashara 170 kutoka Nigeria ambao wamehudhuria
sherehe hiyo kama wageni wa Alhaj Dangote.

Picha – Kiwanda cha Saruji Mtwara
Ujumbe wa Dangote Group umeongozwa na
Mh. Mallam Nasir Ahmad El Rufai, Gavana wa Jimbo la Kaduna ambaye pia
ameiwakilisha serikali ya Nigeria ambayo imekuwa inawaasa
wafanyabiashara wake kusambaza uwekezaji wao katika Bara la Afrika na
hasa katika nchi zenye utulivu wa uhakika kama Tanzania.
Kiwanda hicho kipya pia kinatarajia
kuajiri watu 1500 katika ajira za moja kwa moja na watu 9000 watapata
ajira zisizokuwa za moja kwa moja.
Kiwanda hicho kitazalisha tani za ujazo milioni tatu kwa mwaka kimegharimu dola za kimarekani milioni 600, ikiwa ni uwekezaji mkubwa zaidi kutoka nje kuingizwa katika uchumi wa Tanzania.
Kiwanda hicho kitazalisha tani za ujazo milioni tatu kwa mwaka kimegharimu dola za kimarekani milioni 600, ikiwa ni uwekezaji mkubwa zaidi kutoka nje kuingizwa katika uchumi wa Tanzania.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment