January 09, 2016

kino 
Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imeahirisha Uchaguzi wa Umeya uliotakiwa ufanyike leo kwa madai ya Zuio la Mahakama ya Kisutu lililotolewa jana jioni likitaka uchaguzi huo usifanyike leo.
Akizungumza na Waandishi wa habari Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni Bwana Aron Kagurumjuli amewaambia waandishi wa habari kuwa aliamua kuahirisha uchaguzi huo baada ya kupokea Zuio la Mahakama lililomfikia asubuhi ya leo likimtaka kusitisha mara moja kwa mchakato wa maandalizi ya Uchaguzi wa Umeya bila kufafanua sababu za pingamizi hilo kufika ghafla wakati wajumbe tayari walikwishafika katika eneo la uchaguzi.
Kuahirishwa kwa uchaguzi huo wa Umeya ambao ungeambatana na kuapishwa kwa Madiwani wa Wilaya ya Kinondoni kumepokelewa kwa mtazamo tofauti na upande wa Upinzani ambao unatafsiri hali hiyo na hujuma na kuahidi kutafakari uwezekano wa kulifikisha suala hilo mahakamani ili kuhakikisha haki inatendeka katika Uchaguzi huo.
Wajumbe na wagombea umeya kupitia vyama pinzani vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA walifika manispaa ya Kinondoni pamoja na wafuasi wao waliokuwa nje ya jengo hilo la manispaa wakishangilia lakini shangwe hizo zilizimwa na taarifa za kuahirisha uchaguzi huo.

Related Posts:

  • Brand New Song: Zombie President - R I P Ngwair   Mwanamuziki na Mtangazaji Maarufu kutoka mkoani Morogoro MC Calvin Maarufu Zombie President, ameachia wimbo wake mpya kabisa uitwao R I P Ngwair. Wimbo wa R I P Ngwair ni wimbo unaoonesha mapenzi ya wazi kabisa k… Read More
  • Audio: Simanzi - CN Record Huu hapa ni wimbo mwingine wa Maombolezo kufuatia ajali ya Roli la Mafuta Msamvu Morogoro iliyopoteza uhai wa zaidi ya watu 75 … Read More
  • Klabu Bingwa Afrika,Yanga yasonga mbele   Klabu ya YANGA imefuzu hatua ya pili ya Klabu Bingwa Afrika baada ya ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Towship Rollers ya Botswana. Bao la Yanga SC limefungwa na Juma Balinya ka… Read More
  • Never Forget Moro - Hoodbangerz Kufuatia tukio la ajali ya Moto uliosababishwa na Roli la Mafuta na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 75 mkoani Morogoro, tukio lililotokea 10 August 2019 siku ya Jumamosi katika eneo la Msamvu, wasanii wa Hood Bangerz … Read More
  • Kombe la Shirikisho Afrika, Azam kanyaga twende   Klabu ya Azam imefuzu hatua ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fasil Kenema ya Ethiopia katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Chamazi Complex, Dar es Salaam. Mabao ya Az… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE