February 26, 2016

Tokeo la picha la lukuvi

Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Wiliam Lukuvi ameagiza kupimwa na kutolewa kwa hati za kimila kwa wananchi wa wilaya ya Mvomero sambamba na kuheshimiwa na kutambuliwa kwa hati hizo na taasisi mbalimbali za kifedha ikiwemo mabenki.
 
Waziri Lukuvi amesema hayo baada ya kufika wilayani Kilosa na kupokea taarifa ya usuluhishi wa migogoro ya ardhi katika kijiji cha Mabwegere wilayani Kilosa,kazi ambayo awali alimwagiza  aliyewahi  kuwa mkuu wa mkoa wa Morogoro Steven Mashishanga kuifanya,ambapo pia ametembelea wilaya ya Mvomero akiwa na timu ya wataalamu wa kuhakiki mipaka ya vijiji sita vya wilaya hiyo na kupima,ambapo amekuwa ni waziri wa tatu kutembelea wilaya hiyo ndani ya kipindi kisichozidi wiki moja,na ametumia fursa hiyo kuzungumza na baadhi ya makundi ya wakulima na wafugaji pamoja na viongozi,na kutoa hati milki za kimila zaidi ya elfu saba,akitaka zitambuliwe.
 
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dr.Rajab Rutengwe amevitaka vyombo vya usalama kutogeuka sababu ya migogoro ya ardhi katika wilaya za mkoa huo,sambamba na kuahidi kubadili viongozi wa jeshi la polisi hususani wilayani Mvomero ili kubadili utendaji,ambapo mkuu wa wilaya ya Mvomero Elizabety Mkwasa akabainisha wapo baadhi ya wafugaji wanaoshiriki katika kukuza migogoro wilayani humo ikiwemo kwa kuruhusu uingizaji wa mifugo kiholela na kutumia watoto kuchunga bila tahadhari.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE