
Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL), imeendelea leo kwa michezo kadhaa huku mchezo
ulikuwa ukitazamwa na mashabiki wengi wa soka ni kati ya Azam iliyokuwa
mwenyeji wa Yanga katika mchezo ulicheza katika Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaa.
Mchezo huo umemalizika kwa sare ya goli mbili kwa mbili.
Azam
ndiyo ilikuwa ya kwanza kuona lango la Yanga dakika ya 12 baada ya beki
wa Yanga, Juma Abdul kujifunga dakika ya 12 na dakika ya 28 beki huyo
akaisawazishia Yanga baada ya kupiga shuti kali lililomzidi nguvu goli
kipa wa Azam, Aishi Manula.
Yanga
ilifanikiwa kupata goli la pili kupitia kwa Donald Ngoma katika dakika
ya 41 baada ya kuunganisha kwa kichwa krosi kutoka kwa Amissi Tambwe
goli lililodumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili dakika ya 70, John Bocco aliiandikia Azam goli la 2 na hadi mchezo huo unamalizika, Azam 2 na Yanga 2.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment