Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limepitisha majina ya wachezaji
wanne wapya wa Yanga, kipa Benno David Kakolanya, Hassan Hamisi Ramadhan
‘Kessy’, Vincent Andrew Chikupe na Juma Hassan Mahadhi kucheza Kombe la
Shirikisho.
Wachezaji hao wamesajiliwa kwa lengo la kuongeza nguvu kwenye kikosi
hicho ambacho kimeingia kwenye hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho
na wanatarajiwa kuanza kukipiga kwenye mechi ya kwanza ya kundi A dhidi
ya Mo Bejala itakayopigwa nchini Afrika Kusini.
Yanga kwa sasa wameweka kambi nchini Uturuki pamoja na nyota hao wanne wakiwa tayari wameshaingia kwenye mipango ya Kocha Mkuu Mholanzi Hans Van De Pluijm akisaidiwa na Juma Mwambusi
Yanga kwa sasa wameweka kambi nchini Uturuki pamoja na nyota hao wanne wakiwa tayari wameshaingia kwenye mipango ya Kocha Mkuu Mholanzi Hans Van De Pluijm akisaidiwa na Juma Mwambusi
0 MAONI YAKO:
Post a Comment