July 24, 2016

Mtunzi: Enea Faidy


..Mwalimu John alipelekwa makuburini kwaajili ya mazishi ingawa yeye alijiona yuko hai. Dorice alikuwa njiani baada ya kutoroka shulen, na alipofika kwenye kijito kidogo alishtushwa na kishindo kikali.
 
Eddy alifikia hatua ya Mwisho kutaka kufanya mapenzi na Doreen lakini kabla ya kufanya hivyo aliachia yowe Kali.

SONGA NAYO UJUE KILICHOJIRI....
....VIJANA wanne wenye nguvu walinyanyua jeneza alililokuwamo Mwalimu John kisha taratibu walipiga hatua kuelekea kwenye nyumba yenye pembe NNE na kina kirefu kiasi aliyotengenezewa mwalimu John.

Sauti za vilio zilizidi kutia simanzi katika eneo lile LA makaburini. Nyimbo za huzuni zilitawala eneo hili huku kila mmoja akisikitika moyoni mwake.

Ndani ya jeneza hilo mwalimu John alikuwa akihangaika sana kuwaita vijana wale ili wasimzike lakini katu hakusikika. 

Alizidi kupiga kelele za kuomba msaada lakini ikabaki kuwa kazi bure. Sauti iliyojaa huzuni kuu ya mkewe Monalisa ilizidi kupenya vyema masikioni mwake, hali hii ilizidi kumtia simanzi mwalimu huyo ambaye sasa alikuwa amekata tamaa ya kuishi tena.

"Daah Doreen hafai" alijisemea mwalimu John huku machozi yakimtiririka kwa kasi kwani bado alikuwa haamini kama kweli anazikwa akiwa mzima.Vijana wale walilishusha jeneza lile lenye mapambo ya kupendeza ndani ya kaburi kisha wakatulia kidogo ili mchungaji atupie neno La mwisho.

Mchungaji alichukua udongo kidogo na kusogelea vyema kwenye shimo alilowekwa mwalimu John."Uliumbwa kwa mavumbi hakika utarudi mavumbini, Bwana alitoa Bwana ametwaa jina La Bwana lihimidiwe... " Mchungaji aliyasema maneno hayo kwa huzuni kisha akaumwaga kaburini udongo ule aliokuwa ameushika mkononi.

Mwalimu John aliyasikia vyema maneno hayo yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wenye sumu. Hakika mwalimu John alikiri kuwa kweli duniani kuna watu na viatu, Doreen alikuwa kiatu chakavu kisichofaa kuvaliwa hata na kichaa.

Vijana walishika vyema sepetu zao ili waanze kutupa udongo kaburini na kumzika mwalimu John lakini kabla hawajaanza kutupa udongo, kilizuka kimbunga kikali cha ghafla kilichofanya watu wapoteane. Jeneza likafunuka ghafla mwalimu John akainuka kutoka kwenye jeneza.


Itaendelea wiki ijayo

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE