October 28, 2016

WAZIRI wa mambo ya ndani ya nchi na mwananchama wa Yanga, Mwigulu Nchemba amefanikiwa kumshawishi kocha mholanzi Hans Van Pluijm arejee katika kazi yake ya kukinoa kikosi cha mabingwa hao watetezi wa Ligi kuu.

Pluijm aliwasilisha barua ya kujiuzulu baada kupata taarifa ya kuwasili kwa kocha wa Zesco ya Zambia, George Lwandamina huku ikidaiwa kufanya mazungumzo na vigogo wa wanajangwani hao bila yeye kupewa taarifa yoyote.



Uongozi wa Yanga umemwandikia Pluijm barua ya kukataa ombi lake la kujiuzulu huku ikimtaka arejee kazini mara moja kuendelea na majukumu yake.

Nchemba alifanya vikao kadhaa na Pluijm na mwisho amefanikiwa kukamilisha adhma yake ya kuona kocha huyo aliyeipa ubingwa Yanga mara mbili mfululizo anabakia kukinoa kikosi hicho.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE