November 30, 2016

11 
Aliyekua mgombea Ubunge  wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Jimbo la Mvomero mwaka 2015, Mchungaji wa kanisa la Assemblies of God, Oswald Mlay na wenzake wawili wameamua kurejea chama cha mapinduzi (CCM) kwa kile walichodai kuridhishwa na kasi ya utendaji kazi wa Rais Dkt. John Magufuli.

Akizungumza na katibu wa mkoa wa chama cha mapinduzi mkoa, Kulwa Milonge, Mchungaji huyo amesema kuwa kwa ridhaa yake mwenyewe ameamua kurejea chama cha mapinduzi kwa kuwa kina sera nzuri na zinazotekelezeka.
“Ninawashukuru kwa kunipokea, mimi ni mfanyakazi nakipenda chama na nina nguvu na ntashilikiana na wananchi wenzangu wa chama cha mapinduzi. Kwakweli niseme Rais Magufuli anafanya kile nilichokuwa nakitaka vile nilivyokuwa navitaka amevifanya na vimeshapitiliza. Kwahiyo sina sababu ya kuwa mnafki kuwa mpinzani na kumuacha mtu kama Rais Magufuli awe peke yake. Kwahiyo narudi nyumbani naomba mnipokee. Katibu ntafanya kazi popote utakapoona nafaa kwa mawazo ushauri kwaajili ya chama chetu,” alisema Mlay.
Wengine waliohamia CCM ni Paul Mboji na Patrick Ambi
Hivi karibuni, Mbunge wa zamani wa NCCR Mageuzi, Moses Joseph Machali alihamia CCM huku naye akidai kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Magufuli.

Related Posts:

  • Mchinjaji wa IS 'Jihadi John' atambuliwa   Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza. Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Moham… Read More
  • Waliomuiba Albino Pendo Wakamatwa Mwanza   Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo, amesema watu wote waliohusika ‘kuiba’ mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (albino) Pendo Emmanuel (4) katika kijiji cha Ndami wilayani Kwimba, Mwanza, wamekamatwa. … Read More
  • Chidi Benzi aikwepa miaka miwili jela   MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imemwachia huru mwanamuziki Rashid Makwilo 'Chid Benz' baada ya kulipa faini ya shilingi laki tisa sh:900,000/=.  Awali Chidi Benzi alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela… Read More
  • Tp Mazembe yasajili watatu    Kikosi cha TP Mazembe cha Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo  Timu ya TP Mazembe ya Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo imewasajili wachezaji watatu wapya toka kwenye timu ya taifa ya Ivory Coast. Nyota … Read More
  • New Audio: Ally Kiba - Chekecha cheketua Baada ya kufanya poa ndani na nje ya Tanzania na wimbo wake wa mwana, Mwanamuziki Ally Kiba sasa amekuja na ngoma yake mpya kabisa inayoitwa Chekecha cheketua. … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE