June 19, 2017

 
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU, imewapandisha kizimbani watu wawili James Rugemalila na Harbinder Seth Sigh kwa tuhuma ya kesi ya Uhujumu Uchumi Katika sakata la ESCROW NA IPTL baada yakufanyika kwa uchunguzi wa muda mrefu.
Watuhumiwa hao ni Mmiliki wa kampuni ya VIP Engineering and Marketing, James Rugemalira na Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Ltd IPTL, Habirnder Seth mwenye asili ya bara la ASIA  wamesomewa mashtaka sita ya uhujumu uchumi katika mahakama ya kisutu jijini Dar es Salaam.
Akisoma mashtaka mbele ya mwendesha mashtaka Poul Kadushi, Wakili wa PCCB Joseph Ihula amesema, mnamo tarehe 18 Octoba mwaka 2011 na tarehe 19 March 2014 matika maeneo mbalimbali nchini Tanzania, Kenya, Afrika kusini na India watuhumiwa hao walitenda kosa la kufanya udanganyifu na kujipatia pesa Katika, shtaka la pili watuhumiwa hao wanakabiliwa na kosa la kujihusisha na uhalifu kwa kushirikiana na baadhi ya watumishi wa umma, na shtaka la tatu na la nne yanayomkabili mtuhumiwa wa kwanza Habirnder Seth ni pamoja na kugushi cheti cha usajili na kutoa nyaraka za kugushi kwa msajili wa makampuni.
Shtaka la 4 na 5 yanayo wakabili watuhumiwa wote wawili nikujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu kiasi cha zaidi ya Dola za kimarekani Milioni 22 na kiasi kingine cha pesa za kitanzania Bilioni 309 za kitanzania pamoja na kuisababishia serikali hasara ya kisi cha Bilioni 309 za kitanzania.
Upelelezi wa shtaka hilo haujakamilika na watuhumiwa wote wamerudishwa mahabusu ambapo kesi yao itatajwa tena tarehe tatu mwezi wa saba mahakamani hapo.
Awali kabla watuhumiwa hao kupandishwa kizimbani, Mkurugenzi wa TAKUKURU Bwana Valentino Mlowola amewaambia waandishi wa habari kuwa mara baada ya kukamilika kwa taratibu za kimahakama kesi hiyo itahamishiwa katika mahakama ya kushugulikia makosa ya uhujumu uchumi maarufu kama mahakama ya mafisadi.

"Leo tunawapa taarifa kwamba tunawafikisha Mahakamani watuhumiwa wawili bwana Harbinder Singh Sethi na James Rugemalila na hawa tuna wafikisha Mahakamani kwa kosa la uhujumu uchumi na makosa mengine yanayo hayo kwa muda mrefu sana nimekua naulizwa kesi za ESCROW na IPTL imeishia wapi, kama tulivyosema mwanzo kwa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na kuzuia rushwa na makosa ya ufisadi,” alisema Mlowola.
Aidha Bw. Mlowola ameongeza kwamba  “Nataka nitoe wito kwa Watanzania kwamba serikali ina nia nzuri na dhati ya vitendo vya kuhujumu uchumi wa nchi yetu ili wananchi wapate maisha bora zaidi na jukumu hili TAKUKURU tutaendelea kulitekeleza kwa nguvu zetu zote kwa weledi wetu wote na kwa umakini wa hali ya juu na kuhakikisha kwamba vitendo vyote vya kuhujumu uchumi vinadhibitiwa ili wananchi wapate maisha bora”.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE