June 24, 2017

 

Serikali ya China imetangaza habari ya kufukiwa watu 140 katika maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kali katika maeneo ya kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Taarifa iliyotangazwa leo na China imesema kuwa, maporomoko ya ardhi yametokea katika mkoa wa Sichuan ambapo jumla ya nyumba 40 ambazo walikuwa wanaishi ndani yake watu 140 zimefukiwa na udongo. Kwa mujibu wa habari hiyo, wafanyakazi wa kutoa misaada wametumwa kwenda eneo hilo na kuanza kutafuta miili ya wahanga wa ajali hiyo.Siku chache zilizopita, mamlaka ya hali ya hewa kwa kushirikiana na idara ya kukabiliana na mafuriko na majanga ya kimaumbile nchini China sambamba na kuonya juu ya hali hiyo, zilitangaza kuwepo uwezekano wa kunyesha mvua kali katika maeneo tofauti ya nchi hiyo yakiwamo ya kusini magharibi. Aidha mvua ambazo zimekuwa zikinyesha katika miezi ya Mei, Juni na Julai zimekuwa zikisababisha hasara kubwa za mali na roho hususan katika maeneo ya kusini mwa nchi.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE