Wakazi wa Kata ya Rudewa wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro wakiwa makini kumsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo Mbraraka Ba Waziri wakati alipokua akifanya mkutano na wananchi hao akiskiliza kero na kutoa utatuzi kwa baadhi ya kero hizo
Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mbaraka Ba Waziri akihutubia wakazi wa vijiji na kata ya Rudewa wakati wa mkutano na wananchi hao alipokua akisikiliza kero na kutoa utatuzi wa kero hizo ikiwemo katika sekta ya Afya, Elimu na Maji.
Mbunge wa jimbo la
Kilosa Mbaraka Ba Waziri akimpa mkono diwani wa kata ya Rudewa Subiri
Joseph wakati akikabidhi mradi waujenzi wa kisima cha mita 100 kwaajili
ya kutatua kero ya maji katika kijiji hicho kulia ni katibu wa CCM
wilaya ya Kilosa Aziza Juma kushoto Hassan Mkopi Mwenyekiti wa
Halmahauri wilaya ya Kilosa pamoja na viongozi mbalimali wa CCM na
serikali.
Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mbaraka Ba Waziri akihutubia wakazi wa vijiji na kata ya Rudewa wakati wa mkutano na wananchi hao alipokua akisikiliza kero na kutoa utatuzi wa kero hizo ikiwemo katika sekta ya Afya, Elimu na Maji.
Diwani wa kata ya Kimamba Pendo
Mpoto akihutubia wananchi wa kata ya Rudewa wakati wa mkutano wa Mbunge
wa Jimbo la Kilosa Mbaraka Ba Waziri alipoku akiongea na wananchi
kuhusu matatizo mbalimbali ya nayo wakabili sambamba na kutoa msaada wa
vifaa kwaajili ya utatuzi wa kero za Maji Elimu na Afya
Mbunge wa jimbo la
Kilosa Mbaraka Ba Waziri akikabidhi diwani wa kata ya Rudewa Subiri
Joseph moja ya mfuko wa simenti kama mfano kwaajili
ya ujenzi wa madarasa ya shule katika kijiji cha Rudewa Kata ya Rudewa
Walayani Kilosa ambapo alitoa msaada wa simenti 200 kwaajili ya shughuli
hiyo.
Mbunge
wa jimbo la Kilosa Mbaraka Ba Waziri ametoa msaada wa ujenzi wa kisima
kikubwa cha mita 100 ambacho kitakuwa na uwezo wa kuhudumia zaidi ya
vijiji viwili katika kijiji cha Rudewa kilichopo kata ya Rudewa wilayani
Kilosa ambapo ujenzi wake umeanza mara moja, kutokana na changamoto ya
upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kuwa tatizo sambamba na
ahadi ya ujenzi wa kituo cha afya kwaajili ya huduma ikiwemo ya
wajawazito pamoja na watoto huku tayari akiwakilisha bati 120 waajili
ya ujenzi wa kituo cha afya simenti 200 kwaajili yakujenga vyumba vya
madarasa ya shule ya msingi Rudewa katika wilaya ya Kilosa.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment