April 25, 2013

Mfalme  na wanae

      Siku   ya  jana  tarehe 24/4  mfalme  wa  Rhyme  Tanzania  Mfalme  Sele,  aliadhimisha  umri wake  wa  kuzaliwa. Hakuipitisha  bure,  tazama  alichokisema  na  kukupa  zawadi  wewe  mdau  wake.

    Jana nimetimiza miaka 37, asanteni kwa kunitakia kheri/furaha na dua zenu njema kwangu kwa Mungu katika siku yangu ya kuzaliwa. Katika ujio huu wa umri na siku zangu za kuishi zinapungua! Kama tunasherekea siku ya kuzaliwa tukumbuke kuna siku ya kufa vilevile, siku ya kuzaliwa iwe changamoto kwetu sote kwa kutathimini sababu za uwepo wetu duniani na kusudio la muumba wetu kutuumba wanadamu, na si wanyama, ndege, wadudu au samaki. Lakini tujifunze kuwa maisha(kuishi) ndio zawadi kubwa pekee aliyotupa Muumba wetu. Tuyatunze maisha yetu na ya wengine kwa kutenda HAKI bila kikomo. HAKUNA ALIYEMKAMILIFU CHINI YA JUA, DUNIA AIHITAJI WAKAMILIFU INAHITAJI WATU WA KWELI. Zawadi yangu kwenu katika ujio huu wa umri ni huo wimbo DINI TUMELETEWA ..... MUNGU AWABARIKI SANA.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE