October 13, 2014

kiba n diamond 
Diamond na Alikiba ndio wasanii wa bongo fleva wenye timu mbili kubwa za
 mashabiki waliogawanyika na kuwashindanisha kwa niaba yao, 

Team Diamond v/s Team Alikiba, 
ushindani ambao umevalishwa ‘mask’ za ‘beef’ ambayo Nasib Abdul 
amedai kuwa haipo.

 ushindani ambao umevalishwa ‘mask’ za ‘beef’
 ambayo Nasib Abdul amedai kuwa haipo.
Platnumz ambaye alikuwa bado hajaamua kuzungumzia tofauti hizo 
ameamua kufunguka juu ya ushindani pamoja na ‘beef’
 iliyokuwa inazungumzwa baina yake na muimbaji huyo wa ‘Mwana’.

 “Nimekua nikiskia muda mrefu vimezungumziwa sana,
 kwenye mitandao katika nini, 
sijui kwanini vinazungumziwa hivyo” aliiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm 

“Unajua kuna time ikifika inabidi uangalie na kuna vitu uvizoee tu 
sababu havikuanza leo hivi vitu sio tu kwa Ali, 
ukiwa unafanya vizuri ni msanii yeyote ambaye atakuwepo nae 
anafanya nyimbo au akatoa nyimbo 
yaani utakuja utashindanishwa nae tu,
Atakuja huyu na huyu na huyu, 
lakini wewe mwenyewe tu kuangalia heshima yako iko wapi 
kuangalia kazi zako unazifanyaje ubora wake”.

 “Tangia mwanzo yaani inavyoanza ishagatokeaga hivyo
 ilikua sijui kwa Belle 9, ilitoka kwa Belle 9 
ikaja nafikiri sijui Sam Wa Ukweli ilikua,
 ikaja sijui kwa Bob Junior,
ikaja pia kwa Ali, ikatoka kwa Ali tena ikaja ikaondoka ikaenda 
kwa Omary 
I mean Ommy Dimpoz, ikatoka tena ikaja kwa Richard Mavoko, 
so kila time inavyokuwa inaenda unafanya vizuri
 hivyo vitu vinakua vinatokea,
so ni we mwenyewe kuangalia na watu wasiokuwa na upeo
 wanaweza wakahisi hawa watu wana tatizo kumbe si tatizo 
ni vitu ambavyo vitakuwepo tu 
kwasababu mashabiki wana tabia wakiona mtu
 anafanya hichi na we unafanya kitu mkiwa katika kazi
 inayofanana hivyo vitu vitatokea yaani watu watashindanisha, 
unaweza hata ukashindanishwa 
na mtu ambae hata hakufikii kiwango kabisa”.

 “Hata kwenye boxing ipo, ukiangalia hata kuna kipindi 
ilikuwa TMK na East Coast,
 ilikuwaga kwa Dully na T.I.D 
hivi ni vitu vya kikazi hata kwenye mpira ndio maana
 kuna Simba na Yanga, lakini haimaanishi 
Simba na Yanga nimaadui wakikutana Ngassa 
ntakupiga ngumi au flani ah ah..”

Diamond amesema kuwa kama Alikiba alikuwa na
 tatizo na yeye anaamini angeweza kumfata na 
kumwambia sababu amefahamiana nae kabla hajakuwa
 mwanamuziki.

 “Sasa hivi yaani karibia mwaka wa tano, 
Mi tangia nianze kufanya 
muziki sijawahi kudrop kila siku nazidi kupanda juu…
so hivyo vitu lazima vitatokea lazima nivikubali, 
inawezekana we unasema we unasema we hauna tatizo
 lakini mwenzio akawa anahisi wewe una tatizo nae, 
lakini naamini kama angekuwa anahisi kama mimi nina
 matatizo na yeye angenifata akaniambia kwa sababu
 mimi sijajuana na Ali kwenye muziki,
Nimejuana na Ali kabla sijakuwa mwanamuziki, 
nimemjua Ali 
kupitia dada yangu Queen Darleen so alikuwa ana 
uwezo wa 
kunifata akaniambia personally kwamba bana 
umefanya hichi na hichi na hichi”.

Diamond amemaliza kwa kusema kuwaomba media na 
mashabiki wasifanye ionekane kama wana beef binafsi
 bali wazishindanishe kazi ili kukuza muziki wa Tanzania.
“Ukiniuliza mimi kiundani kabisa siamini kama kutakua 
na tatizola damu ya mtu na mtu,bali ni vitu ambavyo vipo vya kisanaa au vya kimashabiki kwa mashabiki.

 Mi nasisitiza sana media na watu wasitengeneze 
kufanya kama ni matatizo ya mtu na mtu kwasababu 
kisanaa inakua haijengi, 
lakini inapokuwa ni baina ya kazi na kazi inakua inasaidia 
kwasababu inafanya watu wawe na changamoto 
ya kusema 
ngoja nitoe kazi kali ili nifanye kitu kizuri inasababisha muziki wetu ukue.”

Chanzo: Bongo5.com

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE