Maelfu ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Iran leo wameandamana
mbele ya Ubalozi wa Ufaransa mjini Tehran kulaani hatua ya gazeti la
Charlie Hebdo la Ufaransa ya kuchapishwa tena vibonzo vinavyomvunjia
heshima Mtume wa Uislamu Muhammad (SAW).
Waandamanaji hao walitoa nara dhidi ya gazeti hilo na kutaka
kufukungwa balozi wa Ufaransa nchini Iran. Waandamanaji pia wamewataka
maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kuchukua hatua dhidi ya
kitendo hicho cha kishenzi.
Maandamano kama hayo ya kulaani kitendo cha kuvunjiwa heshima Mtume
Mtukufu yameshuhudiwa pia katika nchi mbalimbalii duniani kama vile
Somalia, Pakistan, Niger na Yemen.
Huko Chechniya makumi ya maelefu ya watu wameandamana katika mji
mkuu wa Grozy kupinga hatua ya gazeti la Charlie Hebdo ya kuchapisha
tena vibonzi vinavyomkejeli Mtume SAW. Waandamaji hao walibeba mabango
yaliyokuwa yameandikwa ‘Tunayempenda Mtume Wetu.’
0 MAONI YAKO:
Post a Comment