February 22, 2015

UNICEF: Watoto wengi wametekwa nyara S/Kusini 
 Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNICEF limetangaza kuwa, vijana wengi wadogo wenye umri wa miaka 13 wametekwa nyara huko Sudan Kusini.UNICEF imeeleza katika ripoti yake kwamba, vijana wadogo wasiopungua 89 walitekwa na watu waliokuwa na silaha ambao walipita majumbani kutafuta watoto wa kiume wa zaidi ya miaka 12. Baadhi yao walichukuliwa wakati wakiwa wanafanya mitihani. Matukio hayo yalitokea kwenye kambi katika jimbo la kaskazini la Malakal, ambalo lina maelfu ya watu waliokimbia vita baina ya wanajeshi wa serikali na wapiganaji. Pande zote mbili katika vita hivyo wametuhumiwa kuwa wanatumia watoto vitani. Hivi karibuni Daniel Bekele Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch Kanda ya Afrika alitangaza kuwa, licha ya kuweko ahadi za mara kadhaa za serikali na wapinzani huko Sudan Kusini za kukomesha utumiaji watoto kama askari vitani, lakini pande mbili hizo zingali zinaendelea kuwatumia watoto kama askari.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE