February 25, 2015

 
Jeshi la polisi mkoa wa Morogoro  limewakamata  wahamiaji haramu 13  kutoka nchini  Ethiopia wakiwa kwenye gari ndogo aina Prado  katika kijiji cha Lusanga  Turiani  wilayani Mvomero wakijiandaa kwenda Afrika kusini kupitia mkoani Mbeya .

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro ACP leonard Paul  
akizungumzia  tukio hilo amesema waethiopia hao walitokea nchini Kenya na kupita Handeni na kuingia wilayani Mvomero na walikuwa wakijiendaa kwenda Mbeya kabla ya kwenda nchini Afrika Kusini kutafuta hifadhi.
Jeshi hilo pia linamshikilia dereva wa gari hiyo na wanafanya mawasilinao na idara ya uhamiaji na baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani.
Naye dereva wa gari ndogo aina ya Prado  Musa Edmund  akiongea  huku akionekana kuficha sura yake  anayeshikiliwa kwa kusafirisha waethiopia hao amesema alimpeleka boss wake Arusha njiani wakati anarudi  alikutana na waethiopia hao  mbapo waliomba awasafirishe kwa  makubalinao kuwa  atalipwa shilingi milioni moja hadi kuwafikisha mkoani Mbeya ambapo alilipwa nusu ya gharama hizo kwa makubalino malipo mengine yangefanyika baada kuwafikisha mkoani Mbeya

Related Posts:

  • Morogoro kukata utepe wa Fiesta 2018   TIGO NA CLOUDS TENA: NI VIBE KAMA LOTE. Taa ya kijani imewaka, honi zinasikika kushtua kila dereva aliyekuwa hajakaa mkao wa kusepa, nchi yote inaweka gia ya kusogea mbele, penye kiza nuru imewaka, penye upweke … Read More
  • Kiswahili kuwa Lugha rasmi ya Afrika Kiongozi wa chama cha watetezi wa Uhuru wa kiuchumi (EFF) cha Afrika Kusini, Julius Malema, ametoa wito wa kupitishwa kwa lugha moja itakayotumika barani Afrika, huku akipendekeza lugha ya Kiswahili kuwa lugha hiyo. Ma… Read More
  • Luka Modric Anyakua Mchezaji Bora, Ronaldo Mshambuliaji Bora KIUNGO wa Klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Croatia, Luka Modric amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya akiwafunika Mo Salah wa Liverpool na Cristiano Ronaldo wa Juventus. DATA 17/18 … Read More
  • Breaking News: Misanya Bingi afariki Dunia   Aliyewahi kuwa mtangazaji maarufu sana wa Radio nchini kupitia Radio One Stereo na ITV Dkt. Misanya Dismas Bingi maarufu Misanya Bingi amefariki Dunia. Taarifa za awali zinasema, misanya Bingi amefariki Dunia usiku … Read More
  • Gari la Mbunge wa CHADEMA lashambuliwa kwa risasi   Gari la Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Manyara, Mhe. Anna Gidarya limeshambuliwa kwa kupigwa risasi kwenye matairi ya mbele na nyuma ya ubavu mmoja muda mfupi uliopita akiwa katika kata ya Majengo, Monduli mkoa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE