August 14, 2015

Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Kala Jeremiah akiongea na waandishi wa habari ili kuwaelezea ...

Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Kala Jeremiah akiongea na waandishi wa habari ili kuwaelezea onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015. Pembeni ni Joseph Haule “Professa J”, Juma Kassim “Sir Nature” pamoja na Msagasumu.

 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Joseph Haule “Professa J” akionyesha msisitizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015. 

 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Juma Kassim “Sir Nature” akionyesha msisitizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25.

Tanzania Oyeeeee! Tanzania Oyeeee! ndiyo wasanii hawa walivyokuwa wakitia msisitizo.

 Baadhi ya wasanii watakaowasha moto Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015.

Mwandishi wa habari wa Times Fm, akifanya mahojiano na Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Joseph Haule “Professa J”.
--

Na Mwandishi Wetu.

Wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya na baadhi ya nyota wa Bongo Movie watafanya onyesho la bure Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25.

Wasanii hao wataongozwa na Mbunge wa Mbeya mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Mbilinyi “Sugu” na nyota wengine kama Juma Kassim “Sir Nature”, Joseph Haule “Professa J” na Kara Jeremiah.

Wengine ni watakaopanda jukwaani siku kuanzia saa 8.00 mchana ni Msaga Sumu, Baba Haji na waigizaji nyota wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper na Auntie Ezekiel.

Akizungumza jijini jana, Professa J alisema kuwa sababu kubwa ya kufanya onyesho hilo ni kutoa elimu kwa mashabiki wao kuhusiana na zoezi la upigaji kura kuchagua viongozi bora wan chi hii wataodumu kwa miaka mitano.

Professa alisema kuwa wanataka kutoa mwamko kwa mashabiki wao kushiriki kwa wingi katika zoezi hilo ili kutumia demokrasia yao kumchagua kiongozi wanayemtaka.

“Tumejiandaa vilivyo kutoa elimu, lengo ni kuwahamasisha mashabiki wetu kufanya kile wanachokiona kinafaa ili kutimiza malengo yao ya kikatiba,” alisema Professa J.

Alisema kuwa mbali ya Dar es Salaam, onyesho hilo pia litafanyika katika mikoa mengine mbalimbali.

Akizungumza katika mkutano huo, Nature aliwaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi ili kupata elimu hiyo ambayo wasanii wameamua kuitoa.

“Hii siyo kampeni ya kisiasa, sisi ni wasanii tumeamua kujitolea kufanya kazi ambayo wasanii wengi duniani wameifanya, lazima tutumie kazi yetu kutoa elimu kwa mashabiki ili wajue wajibu wao katika mambo mbali mbali pamoja na uchaguzi mkuu,” alisema Nature

Related Posts:

  • DIAMOND SASA HAWEZEKANI, AINGIA NDANI YA TUZO ZINGINE NIGERIA   @diamondplatnumz yupo nominated kwa tuzo hizi zingine za nchini Nigeria#The_Headies kama #BestAfricanArtiste Kumpigia kura we bonyeza http://hiphopworldmagazine.com/theheadies/vote2014/ then weka screen rot… Read More
  • NEW VIDEO/ HAMJUI - VANESSA MDEE Mwana muziki Vanessa Mdee Veemoney hapa anakupa ruhusa ya kuitazama video yake mpya ya Hamjui, iliyofanyika kwa viwango vya juu sana. hii ni miungoni mwa video zitakazoleta mageuzi makubwa sana ya soko la muziki wetu &nbs… Read More
  • HABARI NJEMA KWA WADAU WA JIMM CARTER Mabadiliko Na Mwonekano Mpya Jimmcarter.com Kuingia mwaka 2015 jimmcarter.com imebadilika mwonekano wake ambao umeboreshwa zaidi kwaajili ya wewe mpenda burudani , NA MWONEKANO WAKE SASA UKO HIVI .SHARE NA RAFIKI UJUMB… Read More
  • AFTER SCHOOL BAS, KIMENUKA UPYA   Ile show kubwa kwaajili ya wanafunzi inayofanyikaga mara moja tu kwa mwaka imerudi tena jumamosi hiiya Tarehe 13 December tunakutana kwenye ufukwe wa escape one Mikocheni kuanzia saa nne kamili Asubuhi  W… Read More
  • YANGA YAIFANYIA UMAFYA SIMBA, WAMSAINISHA MRWANDA USIKU   HABARI zilizotufikia usiku wa kuamkia leo, zinasema kuwa Mshambuliaji wa timu ya Polisi Moro, Danny Mrwanda, amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia Klabu ya Yanga ya jijini Dar es salaam Imekuwa ni … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE