August 21, 2015

Shirika la ugavi wa umeme Tanesco mkoa wa Morogoro limefanya oparation na kuwawakamata watu wanne waliojiunganishia umeme kinyume na sheria katika eneo la Dumila wilaya ya kilosa zikiwemo nyumba za kuishi, kumbi za starehe na kituo cha kuuza mafuta cha Turumba kilichopo Dumila.
Wizi huo wa umeme umebainika kufuatia maafisa wa shirika la umeme Tanesco mkoani hapa kufanya opersheni ya kuwasaka wateja wanaojiunganishia umeme na kusababisha hasara kwa shirika hilo ambapo akizungumza wakati wa operesheni hiyo mhandisi Mposheleye Mwasenga amesema shirika limekuwa likipata hasara na kutokea majanga ya moto katika maeneo mengi nchini kutokana na baadhi ya wateja kuiba umeme.
Aidha mhandisi Mwasenga amesema Tanesco haitasita kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaojihusisha na wizi wa umeme ambapo pia amesema msako huo ni endelevu na kuwataka wananchi kutoa tarifa za watu wanaolihujumu shirika hilo.
Kwa upande wao baadhi ya watuhumiwa wa wizi wa umeme waliokamatwa wamekiri kuhusika na wizi huo ingawa wametupia lawama shirika hilo kulimbikiza ankara za umeme kwa zaidi ya miezi mitatu bila kuwaletea wateja wao hali inayosababisha wateja hao kushindwa kulipa kwa mkupuo mmoja  na hivyo kuamua kujiunganishia ili kuepuka gharama kubwa huku wengine wakikana kuhusika na wizi huo.
Chanzo: itv.co.tz

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE