August 21, 2015

  
Picha hii ni kwa hisani ya Maktaba ya Google
Baada ya kufungiwa na mamlaka ya chakula na dawa kwa machinjio ya nyama ya manispaa ya Morogoro,wachinjaji na wafanyabiashara wa Nyama katika manispaa ya Morogoro wametishia kugoma kuendelea kutumia machinjio ya sasa ya dharura ya dakawa wilayani Mvomero waliyopewa na mamlaka husika,kwa madai kuwa  eneo hilo ni mbali na gharama za ushuru zimeongezeka.
Wafanyabiashara hao wa nyama wamelalamikia kufuata huduma hiyo ya machinjio eneo la dakawa kwa madai ni mbali,na wanalazimika kufuata umbali wa zaidi ya kilometa 80 kwenda na kurudi kutokea mjini sambamba na usumbufu  mwingine,na kwamba hali hiyo imekwenda sambamba na ongezeko la gharama za ushuru,mambo ambayo ni hasara kwao kiuendeshaji na yanachelewesha upatikanaji wa huduma kwa wakati.
 
Mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro Theresia Mahongo,alipohojiwa kuhusiana na hatua hiyo na ile ya kufungiwa na TFDA baada ya ukaguzi wa kushtukiza,amesema wanaendelea vyema na marekebisho na matengenezo ya machinjio hayo yaliyofungiwa ili kukidhi vigezo na kwamba hadi kufikia ijumaa  ya wiki ijayo huenda wakawa wamekamilisha na kuendelea upya kwa shughuli za  sughuli za uchinjaji kama kawaida.
 
Siku ya jumanne wiki hii,mamlaka ya chakula na dawa TFDA ilifanya ukaguzi wa kushtukiza katika machinjio ya manispaa ya Morogoro na kulazimika kuifungia machinjio hiyo kutokana na dosari kadhaa zilizojitokeza,ikiwemo kukithiri kwa uchafu,hali inayotishia usalama wa watumiaji wa nyama,ambapo manispaa iliwataka wafanyabiashara kutumia machinjio ya dakawa wilayani mvomero kwa dharura,lakini baadhi ya wachinjaji wamegomea kwenda kutokana na umbali na sababu nyingine.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE