December 07, 2015


Rais Dk John Pombe Magufuli, ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa wizara ya Uchukuzi, Dk Shaban Mwinjaka pamoja na kuvunja bodi ya bandari na kutengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Bandari Prof Joseph Msambichaka na Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Awadhi Massawe.
Uamuzi huo ni hatua ya Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk John Pombe Magufuli, kuwachukulia hatua watumishi wa taasisi za umma na serikali kutokana na uwajibikaji mbovu na uzembe kazini ulioisabishia hasara ya mabilion ya shilingi serikali .
Miongoni mwa hatua nyingine zilizochukuliwa na Rais Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kasim Majaliwa za kuzuia upotevu wa mapato ya serikali kwenye mamlaka ya Bandari ni kuwasimamisha kazi wale wote waliohusika kupitisha makontena kinyume na utaratibu ambao ni wasimamizi wanane wa Bandari kavu.
Katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akiambatana na katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue anaeleza wengine waliosimamishwa kazi kupisha uchunguzi kuwa nia viongozi wanne wa mamlaka ya Bandari ambao walitoa ruhusa ya makontena kutoka ndani ya bandari kwenda kwenye bandari kavu.
Kuhusiana na shirika la Reli Tanzania TRL juu ya matumizi mabaya ya fedha shilingi bilion 13 nje ya utaratibu, waziri Mkuu Majaliwa amesema licha ya kwamba uchunguzi unaendelea, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Shaban Mwinjaka uteuzi wake umetenguliwa na rais na kwamba atapangiwa kazi nyingine.
Novemba 27 mwaka huu Waziri Mkuu alifanya ziara ya kushtukiza Bandari ya Dar es salaam ambapo alifichua mwanya wa ukwepaji kodi kwa makontena 329 yaliyopitishwa bandarini kinyume cha utaratibu.
Pia Desemba 4 mwaka huu alirudi tena Bandarini akiwa na ripoti ya ukaguzi wa ndani ya Julai 30 2015 ya Mamlaka ya Bandari ambayo ilionesha ukwepaji kodi ikiwemo makontena 2387 yaliyopitishwa kati ya Machi – septemba 2014 kinyume cha utaratibu.

Related Posts:

  • AC Milan Yafungiwa WAKON G­WE wasokanchini Italia, AC Milan wamefungiwa ku­shiriki michuano ya Ulaya kwa mwaka mmoja kuto­kana na kukiuka kanuni za soka. Timu hiyo ilikuwa iki­jiandaa kushiriki katika mi­chuano ya Europa League msimu u… Read More
  • Official Music Video: Totoa - Aslay   Aslay, tayari kabisa leo hii amekuletea video ya wimbo wake wa Totoa. Bofya hapa chini kuutazama                    … Read More
  • Vanessa na Jux wafanya kufuru Mtwara                             Umati wa mashabiki uliojitokeza kwenye tamasha hilo.  T… Read More
  • Bei ya Jezi ya Ronaldo Juve ni hii hapa Rasmi Cristiano Ronaldo ajiunga na Juventus ya Italia  Imekuwa ni wiki yenye furaha kwa Mreno, Cristiano Ronaldo baada ya kuvuta mkwanja mrefu  kutoka klabu ya Juventus wakati mashabiki wa vibibi hao wa Turi… Read More
  • CUF yajitoa rasmi, waipa nasaa UKAWA Chama cha wananchi CUF, Kimetangaza rasmi kujitoa katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa marudio unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao nchini. Akitoa taarifa kwa umma Naibu Mkurugenzi wa Habari , Uenezi na Mahusiano ya Umma wa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE