December 18, 2015

 
 Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Mama Anna Mghwira amesema endapo serikali ingeelekeza nguvu zake kwenye uzoaji taka, zingeweza kuongeza ajira kwa kutengenezwa viwanda ambavyo vitatumia taka hizo katika uzalishaji wa bidhaa

Akizungumza na East africa Radio Mama Anna amesema kuwa kwa nchi nyingine taka ni mali ambapo zinaweza kutengeneza viwanda zaidi ya vitatu ambavyo vinaweza kutoa ajira na kukuza uchumi wa nchi.
Mama Anna ameongeza kuwa endapo fedha zilizotengwa kwa ajili ya shughuli ya Uhuru zingetumika katika uwekezaji wa takataka hizo ikiwemo kutengeneza madampo makubwa ya kuhifadhia taka hizo ambazo zinaweza kutumika katika shughuli tofauti za kuliingizia taifa kipato.
Mwenyekiti huyo wa ACT amesema takataka hizo zinaweza kutengeneza viwanda vya chuma, chupa, mbolea, karatasi ambapo wajasiriamali wanaweza kupata fursa ya kuwekeza katika maeneo hayo.
Aidha amesema tatizo la uchafu katika majiji nchini kubwa ambapo unahitajika mpango maalum wa kuweza kuyasafisha ili kuitoa Tanzania kutoka katika nchi yenye majiji machafu kuelekea kwenye hali ya wastani ya usafi.

Related Posts:

  • Kenyatta atangaza siku tatu za maombolezo Kenya Rais Uhuru Kenyatta Wa Kenya ametangaza siku 3 za maombolezo na bendera kupepea nusu mlingoti kufuatia shambulio la kigaidi dhidi ya Chuo Kikuu cha Garissa lililoua karibu watu 150. Akilihutubia taifa kutoka Ikulu ya Nairobi… Read More
  • Christian Bella Kuleta Mapinduzi ya Muziki wa Dance Inchini Tanzania Mfalme wa Masauti Christian Bella ameachia Track yake mpya Nashindwa Audio pamoja na Video, Audio ya wimbo huo imefanywa chini ya Studio za Combination sound chini ya Producer man Walter na Video imefanyika Africa ya Kusini … Read More
  • Wapinzanu washinda uchaguzi NigeriaRais mpya wa Nigeria Buhari Muhammadu Buhari, ni Muisilamu, mzaliwa wa Jimbo la Katsina, Nigeria kaskazini. Alizaliwa mwaka 1942, Buhari alikuwa kiongozi wa saba wa taifa la Nigeria, baina ya mwaka 1983-1985. Ni jenerali msta… Read More
  • Al-Shabab watishia kuishambulia tena Kenya Kundi la wanamgambo wa al-Shabab wa Somalia limetishia kuishambulia tena Kenya na kusisitiza kwamba, Wakenya watakabaliwa na vita vya muda mrefu na vya kutisha. Taarifa ya wanamgambo wa al-Shabab imebainisha kwamba, muda sio… Read More
  • WhatsApp yaanzisha huduma ya kupiga simu Mtandao wa kijamii wa whatsapp unautumiwa na mamilioni ya watu ulimwenguni, umeanzisha uduma mpya ya kupiga na kupokea simu Awali mtandao huo ulikua na huduma za kawaida za kutuma ujumbe, video, picha au kurekodi sauti. Kwas… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE