December 18, 2015

 
 Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Mama Anna Mghwira amesema endapo serikali ingeelekeza nguvu zake kwenye uzoaji taka, zingeweza kuongeza ajira kwa kutengenezwa viwanda ambavyo vitatumia taka hizo katika uzalishaji wa bidhaa

Akizungumza na East africa Radio Mama Anna amesema kuwa kwa nchi nyingine taka ni mali ambapo zinaweza kutengeneza viwanda zaidi ya vitatu ambavyo vinaweza kutoa ajira na kukuza uchumi wa nchi.
Mama Anna ameongeza kuwa endapo fedha zilizotengwa kwa ajili ya shughuli ya Uhuru zingetumika katika uwekezaji wa takataka hizo ikiwemo kutengeneza madampo makubwa ya kuhifadhia taka hizo ambazo zinaweza kutumika katika shughuli tofauti za kuliingizia taifa kipato.
Mwenyekiti huyo wa ACT amesema takataka hizo zinaweza kutengeneza viwanda vya chuma, chupa, mbolea, karatasi ambapo wajasiriamali wanaweza kupata fursa ya kuwekeza katika maeneo hayo.
Aidha amesema tatizo la uchafu katika majiji nchini kubwa ambapo unahitajika mpango maalum wa kuweza kuyasafisha ili kuitoa Tanzania kutoka katika nchi yenye majiji machafu kuelekea kwenye hali ya wastani ya usafi.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE