March 15, 2016

               

Na Mwashungi Tahir na miza Kona – Maelezo Zanzibar    

Nyumba ya Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame imeripuliwa  na kitu kinachosadikiwa kuwa  ni bomu na watu wasiojulikana  majira ya saa 5.00 usiku huko Kijichi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Ofisini kwake Makao Makuu ya Polisi Kilimani, Kamishna Hamdani amesema tukio hilo limeathiri sehemu ya paa la nyumba na dari na  kujeruhi baadhi ya watu  waliokuwa wamelala  na kusababisha hasara kubwa.

Amesema tukio hilo linafanana na  lile lililotokea tarehe 03 mwezi huu katika Maskani ya CCM Kisonge Unguja hivyo polisi inaendelea kufanya uchunguzi ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu wanaofanya  uhalifu huo.

Akizungumzia  matukio  mengine ya uhalifu na kuchoma moto nyumba, maskani na kituo cha Afya huko Pemba, alisema  Jeshi la Polisi limeanza msako mkali na kuwatia mbaroni watu 31 ambao wanaendelea kuhojiwa na watakaohusika watafikishwa  katika vyombo vya sheria.

Kamishna Hamdani amewatoa hofu  wananchi kuhusu usalama wao na mali zao kuelekea uchaguzi wa marudio utakaofanyika tarehe 20 mwezi huu na kuwepo kwa ongezeko la askari katika maeneo  mengi ya mijini na vijijini  ni  moja ya juhudi za kuimarisha  ulinzi  na kuhakikisha  uchaguzi huo utakuwa salama na amani.

Ametahadharisha kuwa mtu yoyote atakayejihusisha kuanzisha vurugu au kufanya kitendo chenye ishara ya  uvunjifu wa amani atapambambana na vyombo vya sheria.

Kamishna Hamdani ametoa wito kwa wananchi waliojiandikisha kupiga kura kujitokeza kwa wingi siku hiyo ili waweze kutimiza haki yao ya msingi ya kikatiba bila ya woga  kwani jeshi hilo limejipanga  kuimarisha ulinzi  sehemu  zote.

                  

Related Posts:

  • TASWIRA YA SHOW YA DIAMOND ALL STAR ELIZABETH NEW JERSEY JITIRIRISHE  All Star Club Elizabeth New Jersey Diamond akikamua licha ya show kuchelewa kuanza na wapenzi wa Diamond kushikwa na jazba wakitaka aendelee lakini ikashindika kutokana na muda wa kufunga club kufika.  … Read More
  • MAJAMBAZI YAUA ARUSHA Mwananchi mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja ameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi eneo na Clock Tower jijini Arusha. Majambazi hao walikuwa wakipora kwenye Bureau De Change iitwayo Nothern ambapo mareh… Read More
  • RAY C ALITAMANI PENZI LA KIKONGWE MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amesema kwa sasa hana mpango wa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu, na kama ikitokea basi atamtaka kuwa na miaka kuanzia 60. Akizungumza kat… Read More
  • ALICHOKIANDIKA WAKILI ABERT MSANDO KUHUSU MSIBA WA ZITTO KABWE   Msando Alberto 7 hrs · Sandown, South Africa · To my brother and friend Zitto Kabwe, I cannot imagine the pain you are going through. All I can say is pole sana for Mama's loss. I pray so that Allah give… Read More
  • MKUTANO YANGA MAMBO SAFIIII Mwenyekiti wa Yanga SC - Yusuf Manji akiongea na wanachama wa kwenye Ukumbi wa Bwalo la Poilisi - Oysterbay Mkutano Mkuu wa marekebisho ya baadhi ya vipengele kwenye Katiba ya Yanga umefanyika na kumalizika salama na… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE