Dakta Hassan al-Turabi, kiongozi na shakhsia muhimu wa upinzani nchini Sudan amefariki dunia.
Hassan al-Turabi aliaga dunia jana katika hospitali moja mjini
Khartoum akiwa na umri wa miaka 84. Ripoti zinaeleza kuwa, mwanasiasa
huyo mkongwe nchini Sudan alifariki dunia kutokana na shinikizo la moyo.
Bwana Turabi alikuwa mshirika wa karibu wa Rais Omar Hassan al-Bashir
wakati alipochukua madaraka kupitia mapinduzi lakini wakakosana muongo
mmoja baadaye.
Licha ya umri mkubwa na uzee, katika miaka ya hivi karibuni, kiongozi huyo wa upinzani alikuwa akitiwa mbaroni mara kwa mara na kushikiliwa kifungoni.
Licha ya mashinikizo na kuandamwa mara kwa mara na serikali ya Rais al-Bashir, lakini mwanasiasa huyo hakuacha kumkosoa Rais al-Bashir.
Licha ya umri mkubwa na uzee, katika miaka ya hivi karibuni, kiongozi huyo wa upinzani alikuwa akitiwa mbaroni mara kwa mara na kushikiliwa kifungoni.
Licha ya mashinikizo na kuandamwa mara kwa mara na serikali ya Rais al-Bashir, lakini mwanasiasa huyo hakuacha kumkosoa Rais al-Bashir.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment