March 06, 2016

Watatu wauawa kwa mripuko wa bomu nchini Somalia
Kwa akali watu watatu wameripotiwa kuuawa katika miripuko iliyotokea leo kusini mwa Somalia.
Miripuko hiyo imetokea katika eneo la Bardera mjini Gedo, kusini mwa Somalia ambapo kwa akali watu watatu wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa. Kwa mujibu wa mashuhuda wa shambulio hilo, miripuko hiyo ilitokea katika barabara kuu ambayo mara nyingi hutumiwa na askari wa kusimamia amani wa Umoja wa Afrika AMISOM, kutoka Ethiopia. Inaelezwa kuwa, shambulizi hilo lililokuwa limewalenga moja kwa moja askari hao wa kusimamia amani nchini Somalia, liliwapata raia na kupelekea raia wa kawaida kupoteza maisha na kujeruhiwa. Licha ya polisi kuanzisha uchunguzi wa hujuma hiyo, imelinyoshea kidole cha lawama kundi la kigaidi la ash-Shabab kwa kuhusika na jinai hiyo. Hayo yanajiri katika hali ambayo Mkuu wa Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika eneo la Pembe ya Afrika, Peter de Clercq amesema kuwa, watoto wapatao 60,000 nchini Somalia wanakabiliwa na hatari ya kifo kutokana na uhaba wa misaada ya kibinadamu nchini humo.

Related Posts:

  • Aliyewaua waingereza kunyongwa hadi kufaKitanzi cha kunyongea watu Mahakama ya Malaysia imemkuta na hatia ya mauaji mtu mmoja kwa tuhuma za mauaji ya wanafunzi wawili wa udaktari kutoka nchini Uingereza.Mauaji hayo yanadaiwa kufanyika August mwakajana katika kisiwa… Read More
  • New Song: Navy Kenzo ft Young Dee - Viza Navy Kenzo wakishirikiana na Young Dee wanakuletea ngoma yao Mpya inaitwa VIZA Sikiliza hapa … Read More
  • Mtanzania akamatwa kwa ugaidiUmmul-Khayr Sadir Abdul (19). Vyombo vya usalama nchini Kenya, vinawashikilia wasichana watatu akiwamo Mtanzania, kwa kile kunachodaiwa kutaka kujiunga na kundi la kigaidi la al-Shabaab huko Somalia. Taarifa kutoka kwa Kamish… Read More
  • New Audio/ Ainea - Najuta kupenda Baada ya kufanya poa na ngoma yake ya sinampangoa naye aliyomshirikisha MR. Blue, hatimaye mkali wa muziki wa Bongo fleva toka mkoani Dodoma Ainea ameachi ngoma yake hii mpya kabisa ambayo tayari imeshaanza kufanya poa k… Read More
  • New Video/Team Racers- Tunavuka mipaka  Baada ya kimya cha muda mrefu hatimaye kundi la muziki wa Hip Hop toka mkoani Morogro Team Racers limeachia video yake mpya ya Tunavuka Mipaka. Hip Hop / Trap Song Preformed By TEAM RACERS  Audio Produc… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE