Kwa akali watu watatu wameripotiwa kuuawa katika miripuko iliyotokea leo kusini mwa Somalia.
Miripuko hiyo imetokea katika eneo la Bardera mjini Gedo, kusini mwa
Somalia ambapo kwa akali watu watatu wameuawa na wengine kadhaa
kujeruhiwa. Kwa mujibu wa mashuhuda wa shambulio hilo, miripuko hiyo
ilitokea katika barabara kuu ambayo mara nyingi hutumiwa na askari wa
kusimamia amani wa Umoja wa Afrika AMISOM, kutoka Ethiopia. Inaelezwa
kuwa, shambulizi hilo lililokuwa limewalenga moja kwa moja askari hao wa
kusimamia amani nchini Somalia, liliwapata raia na kupelekea raia wa
kawaida kupoteza maisha na kujeruhiwa. Licha ya polisi kuanzisha
uchunguzi wa hujuma hiyo, imelinyoshea kidole cha lawama kundi la
kigaidi la ash-Shabab kwa kuhusika na jinai hiyo. Hayo yanajiri katika
hali ambayo Mkuu wa Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa
katika eneo la Pembe ya Afrika, Peter de Clercq amesema kuwa, watoto
wapatao 60,000 nchini Somalia wanakabiliwa na hatari ya kifo kutokana na
uhaba wa misaada ya kibinadamu nchini humo.
DIWANI WA KATA YA MSHANGANO AJIUZULU
-
Diwani wa Kata ya Mshangano ,Samuel Mbano akionesha barua ya kujiuzulu
Diwani wa Kata ya Mshangano ,Samuel Mbano aliyejiuzulu kupitia Chama Cha
Mapind...
2 hours ago
0 MAONI YAKO:
Post a Comment