Tetemeko lililotokea mkoani Kagera Septemba 10, limesababisha vifo vya watu 16, kuacha watu 253 wakiwa na majeraha mbalimbali ya mwili na nyumba zaidi ya 1000 zikiwa zimebomolewa.
Taarifa kutoka kwa msemaji wa Rais Kenyatta, Kenua alisema kuwa Rais Kenyatta ameahidi kutoa msaada wa mabati, blanketi na magodoro ili kuwasaidia watu wasio na makazi mkoani Kagera.
Msaada huo utasafirishwa kwa ndege na Jeshi la Kenya Jumanne Septemba 13 hadi mkoani Kagera ambapo ndipo palipopata madhara.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment