October 19, 2016

Siku kadhaa kabla ya kufanyika mkutano wa Yanga, Kamati ya Mwafaka ya Wazee wa Yanga imezungumza na waandishi wa habari kuhusu mfumo ambao mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji anataka autumie katika kuingia mkataba wa miaka 10 kuimiliki nembo ya klabu.
Katibu wa Kamati ya Mwafaka ya Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimalia amesema ambacho Manji anakifanya kinaweza kusababisha timu hiy ikaingia katika vurugu ambazo hazikuwepo kwa muda mrefu kwa sababu njia ambayo anatumia inawagawa wanachama na mashabiki kwa wengine kuutaka mfumo na wengine kuukataa.
“Hatutaki kurudi kule tulipokuwepo katika mgogoro wa miaka saba, mwaka 2003 ndiyo tukapata usuluhisho na kukubaliana kuwa litumike jina ambalo lilikubaliwa na waasisi wetu, tukakubaliana kuwa kuwe na Yanga SC na Yanga Cooperation,
“Yanga kampuni ilifishwa na kukawa na utaratibu kuwa kuwe na hisa, Yanga SC kuwe na hisa 51 na wanachama wawe na asilimia 49, na tulizunguka mikoa mingi ili kufuta mgogoro uliokuwepo na kuomba ridhaa ya wanachama wa klabu kukubali hisa,” alisema Akilimali na kuongeza.
“Tulipata mwenyekiti mpaka anatoka timu ilikuwa na Mil. 200, tukampata bwana Nchunga yeye akajiuzulu baada ya miaka miwili, tukamchagua Bwana Manji akaongoza kwa miaka miwili, kwasababu tu ya upenzi ikabidi tuikanyage katika akaongeza muda, ili tujipange na yeye ajipange ili tutafute kuongozi wa baada yake, na tukafikia hatua ya kumchagua kwa mara nyingine,
“Haijafika hata miezi nane imeibuka swala la deni la Bilioni 11 na laki sita, jambo ambalo limetushtusha sana wanayanga, limekuja tamko la mwenyekiti kuleta hoja kuwa akodishwe Yanga na lebo yake kwa muda wa miaka 10, kwasisi wote tunasema Yanga ni kubwa sana, Yanga haiwezi kukodishwa kama masufuria ya kwenda shughulini. Kupitia mimi na wazee wa kamati tumesema hatukubaliani na hilo”
mohammed-msumi 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga, Mohammed Msumi.
Nae aliyekuwa Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga, Mohammed Msumi amesema kutokana na Manji kuwa na mahitaji makubwa na klabu ni vyema akakaa pembeni na kuanzisha timu yake mwenyewe na kuacha Yanga iendeshwe na mfumo ambao umezoeleka.
“Kwanini anataka hili jambo haraka haraka na wakati alisema Yanga inajiendesha kwa hasara, mfanyaniashara gani anakaa sehemu ya aina hiyo, kama hawezi kufata utaratbu anaweza kuanzisha timu nyingine sio kuitaka yanga na kutumia mamlaka kwa mabavu ili tu aipate Yanga,” alisema Msumi.
Siku kadhaa kabla ya kufanyika mkutano wa Yanga, Kamati ya Mwafaka ya Wazee wa Yanga imezungumza na waandishi wa habari kuhusu mfumo ambao mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji anataka autumie katika kuingia mkataba wa miaka 10 kuimiliki nembo ya klabu.
Katibu wa Kamati ya Mwafaka ya Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimalia amesema ambacho Manji anakifanya kinaweza kusababisha timu hiy ikaingia katika vurugu ambazo hazikuwepo kwa muda mrefu kwa sababu njia ambayo anatumia inawagawa wanachama na mashabiki kwa wengine kuutaka mfumo na wengine kuukataa.
“Hatutaki kurudi kule tulipokuwepo katika mgogoro wa miaka saba, mwaka 2003 ndiyo tukapata usuluhisho na kukubaliana kuwa litumike jina ambalo lilikubaliwa na waasisi wetu, tukakubaliana kuwa kuwe na Yanga SC na Yanga Cooperation,
“Yanga kampuni ilifishwa na kukawa na utaratibu kuwa kuwe na hisa, Yanga SC kuwe na hisa 51 na wanachama wawe na asilimia 49, na tulizunguka mikoa mingi ili kufuta mgogoro uliokuwepo na kuomba ridhaa ya wanachama wa klabu kukubali hisa,” alisema Akilimali na kuongeza.
“Tulipata mwenyekiti mpaka anatoka timu ilikuwa na Mil. 200, tukampata bwana Nchunga yeye akajiuzulu baada ya miaka miwili, tukamchagua Bwana Manji akaongoza kwa miaka miwili, kwasababu tu ya upenzi ikabidi tuikanyage katika akaongeza muda, ili tujipange na yeye ajipange ili tutafute kuongozi wa baada yake, na tukafikia hatua ya kumchagua kwa mara nyingine,
“Haijafika hata miezi nane imeibuka swala la deni la Bilioni 11 na laki sita, jambo ambalo limetushtusha sana wanayanga, limekuja tamko la mwenyekiti kuleta hoja kuwa akodishwe Yanga na lebo yake kwa muda wa miaka 10, kwasisi wote tunasema Yanga ni kubwa sana, Yanga haiwezi kukodishwa kama masufuria ya kwenda shughulini. Kupitia mimi na wazee wa kamati tumesema hatukubaliani na hilo”
mohammed-msumi 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga, Mohammed Msumi.
Nae aliyekuwa Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga, Mohammed Msumi amesema kutokana na Manji kuwa na mahitaji makubwa na klabu ni vyema akakaa pembeni na kuanzisha timu yake mwenyewe na kuacha Yanga iendeshwe na mfumo ambao umezoeleka.
“Kwanini anataka hili jambo haraka haraka na wakati alisema Yanga inajiendesha kwa hasara, mfanyaniashara gani anakaa sehemu ya aina hiyo, kama hawezi kufata utaratbu anaweza kuanzisha timu nyingine sio kuitaka yanga na kutumia mamlaka kwa mabavu ili tu aipate Yanga,” alisema Msumi.

Related Posts:

  • Habari katika magazeti leo hii jumatatu 23 Mei Habari za Jumatatu ya leo ya 23 Mei 2016. Karibu katika kurasa za magazeti ya leo hii tulizokukusanyia katika magazeti mbalimbali ya hapa nchini. Habari kubwa zilizobeba uzito na kuwekwa katika kurasa za mwanzo na za mwis… Read More
  • Meneja wa Trey Songz azungumza haya kuhusu Diamond Platnumz CEO wa kampuni ya KWL Management inayowasimamia wasanii wakubwa wa Marekani wakiwemo Trey Songz na Big Sean, Kevin Liles, amefunguka kwenye Twitter kuhusiana na ukaribu alionao na Diamond. Kupitia session yake ya #… Read More
  •  Kocha wa kilabu ya Manchester United Louis van Gaal hatimaye baada ya tetesi kuwa nyingi sasa rasmi amefutwa kazi kama kocha wa klabu ya Manchester United ,huku aliyekuwa mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho akita… Read More
  • Manchester United kumteua Jose Mourinho kuwa kocha wake mpya   Manchester United wanatarajia kumtangaza Jose Mourinho kuwa kocha wake mpya, BBC Sport imeripoti. Inaaminika kuwa deal hiyo na raia huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 53 ilikubaliwa kabla ya ushindi wa United kw… Read More
  • Alikiba amuombea kura Diamond Platnumz Alikiba alisema haya kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio na kusisitiza kuwa yeye kusaini mkataba na kampuni ya 'Sony Music' jambo kubwa sana katik… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE