August 19, 2017

 
Abuja, Nigeria
Baada ya kukaa takribani miezi mitatu akipatiwa matibabu nchini Uingereza hatimaye Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari amewasili katika mji mkuu wa Abuja na kupokelewa na viongozi wa ngazi za juu wa taifa hilo wakiongozwa na Makamu wa Rais wa nchi hiyo.
Rais Buhari alikuwa katika matibabu kwenye moja ya hospitali nchini humo ambapo alilazwa kwa takriban miezi mitatu. Hata hivyo haijafahamika Rais huyo alikuwa akiugua ugonjwa gani.
Hii ni mara ya tatu kwa kiongozi huyo kwenda Uingereza kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Jumatatu ijayo kiongozi huyo anatarajiwa kuhutubia taifa hilo.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE