November 19, 2017

Mfanyakazi wa hoteli za kitalii za andBeyond Serengeti, Moses Muhina aliyetajwa kuwa ni miongoni mwa abiria waliofariki dunia katika ajali ya ndege ya Shirika la Coastal Aviation, imebainika alibadili ndege muda mfupi kabla ya safari ili kuwahi kazini. Muhina ambaye ni mwongozaji watalii katika hoteli hiyo, alikuwa aondoke na ndege ya Coastal Aviation saa nne asubuhi lakini viongozi wa hoteli walimbadilishia ndege, hivyo aliondoka na Air Exel iliyofika salama Serengeti.

 

Akizungumza na gazeti hili, meneja uendeshaji wa Hoteli ya andBeyond Serengeti Under Canvas, Mussa Matala alisema Muhina ambaye anasomeka kwenye orodha ya ndege kama Maina alikuwa apande ndege hiyo lakini walimbadilishia. Alisema waliomba aondolewe kwenye orodha ya wasafiri wa ndege hiyo lakini kwa bahati mbaya hadi ndege ilipoondoka jina lake lilikuwapo. Wakati huohuo, raia watano wa kigeni ambao walifariki dunia katika ajali hiyo, akiwamo rubani Dewald Raubenheimer raia wa Afrika Kusini, ambaye kwenye orodha ya awali ya waliofariki jina lake halikuwapo anatarajiwa kusafirishwa leo.

             
Mhudumu wa chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya mkoa ya Mount Meru, Francis Costa alisema miili mitatu kati ya 11 imechukuliwa na ndugu zao. Alisema miili iliyochukuliwa ni ya ndugu wawili waliokuwa wakurugenzi wa Masai Wondering, Nasibu na Shatri Mfinanga. Mwingine ni wa Joyce Mkama ambaye alikuwa mfanyakazi wa Hoteli ya Serena. “Uchunguzi wa miili ya wageni kutoka nje ya nchi unaendelea na ukikamilika itasafirishwa kwa mazishi katika nchi za Afrika Kusini, Ujerumani na Italia,”

alisema. Ndege hiyo namba 5H-EGG aina ya Cessna Grand Caravan ilianguka baada ya kugonga kingo za creta ya Empakai, umbali wa mita 3,250 kutoka usawa wa bahari ikitoka Kilimanjaro kwenda Hifadhi ya Serengeti. Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema uchunguzi unaendelea kuhusu ajali hiyo.

Related Posts:

  • Ainea kuja na Juddy wiki hii     Mwanamuziki wa kizazi kipya toka mkoani Dodoma Aine wa sinampango naye, yupo mbioni kuachia ngoma yake mpya ya Juddy aliyomshirikisha Dullayo. Akitia Story na blog hii, Ainea amesema ameamua kuja na Dullayo k… Read More
  • Mainda aanika kinachoua sanaa   BILA kuwataja kwa majina, msanii wa filamu Bongo, Ruth Suka ‘Mainda’ amesema kitendo cha baadhi ya wasanii wanaojiona wamefikia vilele vyote vya mafanikio na kuwafanyia roho mbaya wenzao, ndiyo moja kati ya sabab… Read More
  • AY: awashauri Diamond na Alikiba Rapper Ambwene Yesayah maarufu kama AY ametoa ushauri kwa Diamond na Alikiba kuweka tofauti zao pembeni na kufanya muziki pamoja. AY ametoa ushauri huo baada ya kuulizwa na shabiki kupitia Kikaangoni cha EATV aliyetaka… Read More
  • TFF yamtangaza Boniface Mkwasa kuwa kocha mpya wa Taifa Stars Shirikisho la soka nchini, TFF, Jumanne hii limemtangaza rasmi Boniface Charles Mkwasa kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars. Mkwasa atasaidiwa na Hemed Morocco kutoka Zanzibar. Taarifa hiyo imetolewa na Rais wa TF… Read More
  • Nyimbo zote za Jose Chameleone toka 1999 - 2014 hizi hapa. Enjoy   Mmabo vipi? leo hii tumekupa offer ya wikend. Burudika na nyimbo za Josee Chameleone toka 1999 mpaka 2014. Hii imetokana na kukujali wewe mdau wetu na mdau wa Josee Chameleone  Bofya hapa chini   &… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE